Kama wewe ni mmoja kati ya wale ambao tunaamka asubuhi na kuanza kufikiria tuvae nini, mwishoe tunaishia kuvaa chochote ili mradi tumevaa au kuishia kuchelewa tuendapo kwa sababu tu hatukuwa tumejitayarisha mapema.
Asikudanganye mtu a good & stylish outfit takes time to create, ni wachache sana wenye kipawa cha kufungua kabati na kuweza ku-create outfit inayoeleweka kwa muda mchache wengine tunahitaji muda na kuyafahamu mavazi yetu haswa, leo tunakuletea tips chache za kutayarisha stylish outfit za week nzima, sio tu zinakufanya u-save muda asubuhi lakini pia utaweza kuonekana stylish week nzima.
- Tengeneza Nywele & Kucha Zako

Yes mtauliza afroswagga sasa nywele na kucha zitafanyaje niwe na stylish outfit, well bila nywele na kucha kuwa safi na kutengenezwa vizuri kwa hakika chochote utakachovaa hakitoonekana vizuri, kwahio hakikisha unatumia muda wako kwenda saloon kutengeneza nywele na kucha zako ziwe katika muonekano mzuri.
- Safisha Viatu Na Pochi Zako
Kama ilivyo kwa kucha na nywele ni vizuri pia ukatumia muda wako kusafisha viatu na pochi zako, ni muhimu sana hivi vikiwa visafi ili kuubeba muonekano wako, hasa katika mapochi wengi huwa tunajisahau kuyasafisha. Pochi kama ni ya leather hakikisha umeifuta na inaonekana vyema kama ni ya vitambaa fua ili iwe safi.
- List down occasions you will attend

Baada ya kufanya vyote hivyo, andika week hio unaratiba gani, utaenda wapi na wapi. Hii inasaidia kukufanya ujue vazi gani litafit wapi, oh yes ushawahi kujikuta siku unatakiwa kwenye event fulani lakini kwa sababu tu hukujiandaa mapema unavaa vazi ambalo hata haliendani na event? kuepuka hizi aibu ndogondogo hakikisha unajiandaa mapema kwa kuandika utaenda wapi ili wakati unachagua mavazi ujue lipi linafaa wapi.
- Plan weekly / Day by day outfit
Wakati una plan day by day outfit zingatia vitu hivi vinne
- Msimu – hii inakuja kwa hali ya hewa gani iliyopo / lakini pia inakuja katika fabrics, colors, & patterns zinazofaa kutumika kutokana na hali ya hewa iliyopo
- Occasions – Kama tulivyoelezea juu jua utaenda wapi na kufanya nini hii itakusaidia ku-plan mavazi yanayoendana na uendapo
- Formality – baada ya kujua msimu, occasion sasa uyaandae mavazi yako kutokana na hizo sehemu, kama formal event kama work meeting / meeting na mteja, kwenda kanisani etc, Semi – Formal events na informal event hizi zote unatakiwa kuzilist na kuandaa mavazi yake.
- Activity – hii inaenda bega kwa bega na formality, ukishajua unaenda wapi basi pia utajua unaenda kufanya nini kama unaenda mahali ambapo unajua utakuwa unatembea kwa muda mrefu basi itabidi ubeba viatu vifupi etc.
Baa ya hapo kaa na kabati lako, anza kuchambua nguo moja baada ya nyingine na uplan ipi utavaa lipi na wapi. Cheza na kabati lako na jaribu ku-create mionekano mingine mipya, mix & match, lakini pia usiache kuzijaribu, isije siku ikafika ukazijaribu ukakuta labda kubwa au haikai kama ambavyo uli-imagine itakaaa.
well kama utajaribu hizi tips usisite kutumia hashtag yetu katika mitandao ya kijamii #afroclosetconfidence
Related posts
HOT TOPICS
Happiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/VZ1jH2zJUg
FollowHappiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/689j7Yjcn0
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
Feza Kessy Atuelezea Kuhusu Fashion & Style Zake
Feza Tadei Kessy ni Muimbaji, Muigizaji lakini pia ni mtunzi wa nyimbo lakini pia Fezza ni former beauty queen ambapo mwaka 2005 alikuwa Miss Dar City Centre, Miss Ilala & Miss Tanzania Runner up. Lakini pia alishawahi kuwepo katika Reality Tv Show – Big Brother Africa. Kwa…