Kuwa mgeni mualikwa kwenye harusi kwasasa ni ghali, yaani ukisikia harusi unaweza kutamani Dunia ifunuke uingie, kuna michango kuna manunuzi ya sare, viatu, makeup, nywele, viremba, accessories na vingine vingi tuseme a wedding guest kwasasa inahitaji investment ya haja.
Well unaweza kuwa mgeni mualikwa ukapendeza lakini harusi ikiisha usifilike, leo tunakuletea Tips kadhaa za kuweza kuwa mgeni mualikwa uliyependeza bila ku-break the bank.
- Anzakujiwekeza mara tu unapopata mualiko
Usisibiri mpaka mwishoni ndio uanze kuhangaika pa kupata hela ya michango na mavazi, hakikisha unajua unachokitaka mapema kitaku-cost shilingi ngapi na uanze kujiwekeza mapema.

- Huitaji kununua sare kwa muhusika
Sasa hivi imetokea namna ambavyo wahusika wanauza sare, utakuta kijora cha sh 6000 kinauzwa 15,000 kwao au kitambaa cha 10,000 kinauzwa 30,000 na wanakukatia na meter kabisa 3 au mbili inawezekana wewe mwembamba hizo meter ni nyingi au una mwili zaidi hizo meter ni chache una poteza pesa nyingi. Jua sare take your time kuitafuta kwenye maduka ya vitambaa nunua inayo kutosha alimradi utokee kwenye sherehe umevaa sare yao.
- Huitaji kwenda kushona kwa ma-designer
The pressure is real, siku hizi wenye sherehe wanakwambia kabisa tunafundi wetu au tuna designer wetu mkali anaweza kukushonea, au ukaona fulani alikuwa wedding guest kwa fulani akashona kwa designer basi na wewe uende. Unaweza kutafuta fundi mzuri mtaani ambae hana bei kubwa ukashona vazi lako na ukapendeza.
- Shoes & Accessories
Kumbuka kununua viatu na accessories ambazo utazivaa tena na tena, sio ununue tu viatu ukavaa kwasiku hiohio na kuacha, nunua viatu na accessories ambavyo unaweza kurudia kwenye sherehe nyingine tena, hakikisha rangi za vitu hivi vinaweza kuingilia na sare nyingine nyingi mfano viatu vya silver au see through.
- Makeup
Unaweza kupaka makeup yako simple as wewe ni wedding guest na sio mwenye sherehe, a simple yet nice makeup ambayo huitaji ku-break the bank maana makeup artist nao kwa bei Ma’shallah.
Related posts
2 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More on on that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-ya-kuwa-dazzling-wedding-guest-bila-ya-kufilisika/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on on that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-ya-kuwa-dazzling-wedding-guest-bila-ya-kufilisika/ […]