Wakati tunapitia mitandao mbalimbali tukakutana na story ya mwanadada aliyeingia katika madeni kisa tu ni kutaka kuwa Fashionista katika Instagram, Lissette Calveiro anasema watu walikuwa wakimuona anaishi maisha mazuri na kusafiri sehemu mbalimbali lakini nyuma ya pazia alikuwa ana mikopo na madeni ya $10,000/- sawa na Tsh 22,591,000.00/- Lissette Calveiro “I was shopping…for clothes to take ‘the perfect ’gram”, she told the New York Post.“I was living above my means. I was living a lie and debt was looming over my head.”
Well hii imeturudisha kwa wenzetu na sisi ambao tunapenda kuonekana tumependeza na tunaishi maisha mazuri katika mitandao ya kijamii, inabidi uangalie uwezo wako na wapi unaweza kufikia na wapi huwezi. Unaweza kupendeza on a budget huitaji kuvuka kiwango chako cha pesa au kujirundikia madeni ili uonekane umependeza.
hizi ni tips tulizo kuandalia za namna unavyo weza kupendeza kulingana na bajeti yako
- Ni Aina Gani Ya Mitindo Unapenda?
Kuna aina nyingi za mitindo kunawale wanaopenda kuwa chic, Vintage, Casual, Sexy, Corporate na nyingine nyingi, Hii itasaidia unapoenda kufanya shopping uweze kuchagua mavazi unayo yapenda na kukufanya uyavae kila mara. Kuna watu wengi ambao hawajui styles zao chochote wanacho kikuta wananunua na mwishoe huishia kuwekwa katika kabati bila kutumiwa hii inafanya utumie fedha nyingi katika mavazi ambayo huyatumii.
- Kagua kile ulicho nacho
Tumia muda wako kukagua kile ulichonacho katika kabati nini huna na nini unacho, nini kinafaa kutolewa na kipi kinahitaji kuongezwa hii itasaidia kukufanya uwe na kabati friendly na kutokutumia fedha nyingi kuongeza vitu ambavyo kumbe unavyo tayari.
- Epuka Trends
Epuka trends kwa maana zinakuja na kuondoka, kuliko kutumia pesa yako katika trends ambazo zinakaa mwezi au miezi kisha kupotea ni bora ukanunua basic pieces ambazo zinadumu muda mrefu, vitu kama Jeans, White Shirt’s, T-shirts, Pumps, Blazer etc ambavyo unaweza kuvitumia zaidi ya mara moja kwa namna tofauti na muda mrefu.
- Be Timeless
Kama ambavyo tumesema hapo juu nunua vitu ambavyo vinaishi, Black Pumps, Little Black Dress etc hivi vinaweza kutumika mara nyingi, vinaishi kwa muda mrefu na katika kununua haya mavazi huitaji kununu ya gharama sana kuna mitumba na kuna wale ambao hawarudii mavazi unaweza kuwa unaongea nao na wakakuuzia kwa bei ya chini kulingana na kipato chako.
- Wekeza katika Ubora
wengi huwa tunasema hapana siwezi kununua shirt ya zaidi ya elfu 20,000/- wakati naweza kupata kama hizo kwa elfu mbilimbili, ni kweli zinapatikana lakini je zina ubora? lipi bora kuwa nazo nyingi ambazo zina haribika kwa muda mchache na zimechakaa au bora kuwa na mbili ambazo zinadumu kwa muda mrefu? Unaweza kununua mtumba lakini uwe quality. Always chagua Quality Over Quantity.
- Shop Sales, Clearance, and Off Season
Always kuwa karibu na maduka, wauzaji wengi wa mavazi huwa wana fanya sales, clearance na off season kuuza bidhaa zao kwa bei ya chini. Hii inakupa nafasi ya kununua kitu bora lakini kwa bei ya chini zaidi. hakikisha iko kitu ni timeless unaweza kukivaa tena na tena kwa sababu kama ni trendy hata kama umekipata kwa bei nafuu hakito kaa kwa muda mrefu.
Related posts
6 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Info to that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-ya-kuwa-stylish-huku-ukiendana-na-bajeti-yako/ […]
… [Trackback]
[…] Information on that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-ya-kuwa-stylish-huku-ukiendana-na-bajeti-yako/ […]
… [Trackback]
[…] Information on that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-ya-kuwa-stylish-huku-ukiendana-na-bajeti-yako/ […]
… [Trackback]
[…] Info to that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-ya-kuwa-stylish-huku-ukiendana-na-bajeti-yako/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Info here on that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-ya-kuwa-stylish-huku-ukiendana-na-bajeti-yako/ […]
… [Trackback]
[…] There you can find 12646 additional Info to that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-ya-kuwa-stylish-huku-ukiendana-na-bajeti-yako/ […]