Hili swala huwa linatokea Mara nyingi majumbani kwetu, wengi wanakatazwa au kupewa mipaka ya nini wavae na nini wasivae na wenza wao, hii hutokea pale tu mwenza anapo penda mwenza wake avae Mavazi ya aina Fulani na si ya aina Fulani na ni kutokana na Sababu tofauti, Inawezekana Kuwa ni wivu au kutokupenda aina hio ya Vazi.
Katika kudumisha mahusiano yoyote ni jambo la kawaida kwa wenza kutafuta namna ya kushahabiana, hii ni kwasababu wawili hawa wamaweza kuwa wanatokea kwenye mazingira yenye tabia na imani tofauti tofauti lakini licha ya hivyo hata linapokuja swala la mapenzi na ushabiki katika baadhi ya vitu kamwe hamuwezi kufanana na hii ndio maana halisi ya binadamu hatufanani
huyu anaweza kuwa anapenda hiki hiliihali mwenza wake asikipende ni jambo la kawaida na wala sio dhambi wala kosa mara nyingi busara hutumika katika kutafuta uhiano huo, aidha mmoja akiache kitu anacho kipenda au mwingine ajifunze kukikubali anacho kipenda mwenzie yote hii ni katika kutafuta uwiano na usawa ili mpate kuishi kwa amani na upendo.
Inawezekana ni mambo madogo madogo lakini leo tunalenga katika mavazi na style Swali linakuja je ni sawa kwa mwenzi wako kukuchagulia nini uvae? Je hii haiingilii Uhuru wako binafsi? Come to think si ni kwamba alikukuta ukiwa unavalia Mavazi ya aina hio Kwanini sasa hivi mko Kwenye mahusiano ayakatae na kutaka uvae Mavazi ya aina fulani yanayo mpendeza yeye?
Kwetu tunaona hupaswi kumchagulia mwenza wako mavazi au style, hupashwi kumuwekea mipaka katika kile ambacho yeye anakipenda na umemkuta akikifanya mwisho wa siku mahusiano yanapaswa kuwa katika kupeana uhuru na kuaminiana, unapo mkataza mwenza wako asivae vazi la aina fulani sababu tu wewe unaona wivu au halikupendezi ni kumnyima uhuru wake katika ulimwengu wa fashion na style lakini pia kumsononesha kwa kushindwa kuvaa kile ambacho moyo wake unapenda.
Tupe maoni yako je ni sawa au si sawa mpenzi wako kukuchagulia mavazi?
Related posts
2 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More Information here to that Topic: afroswagga.com/mitindo/ni-sawa-mwenza-wako-kukuweka-mipaka-katika-mavazi/ […]
… [Trackback]
[…] Here you can find 49076 more Information to that Topic: afroswagga.com/mitindo/ni-sawa-mwenza-wako-kukuweka-mipaka-katika-mavazi/ […]