Shindano la Master Tanzania liliweza fanyika mwezi huu kwa mara ya kwanza nchini, na Josh Ipyana
kuibuka mshindi, Master Tanzania 2019. Ili kuweza kumtambua na kulielewa shindano tuliweza zungumza naye:

AFROSWAGGA: Waweza tuelezea Master Tanzania 2019 lililenga kutafuta kijana wa aina gani?
JOSH: Master Tanzania ni shindano linalotafuta kijana,umri wa miaka 18-29 mwenye ujasiri, akili pamoja na kipaji chenye upekee. Kipaji ndo kitu muhimu sana.
AFROSWAGGA: Mshindi wa Master Tanzania 2019 huzawadiwa nini?
JOSH: Wanatafutwa washindi watatu kama 1 st runner up, 2 nd runner up pamoja na Master Tanzania mwenyewe. Washindi watatu wataungana mwisho wa mwezi October kuelekea Hollywood Marekani kwa ajili ya kuendeleza vipaji vyao.
AFROSWAGGA: Kipaji chako kilichokuwezesha kuonekana ni kipi hadi kushinda?
JOSH: Kipaji changu ni muigizaji wa sauti ama voice over artist. And yes, ni mwanamitindo yaani model.
AFROSWAGGA: Pia umekuwa ukifanya unamitindo (modelling). Je ulianza lini? Ulishawishikaje? Na experience yako ya kwanza on the runway ilikuwaje?
JOSH: Nilianza kufanya mitindo mwaka 2017 so now ni miaka miwili hivi. Nilishawishika kwasababu napenda sana mitindo na kilichonitia nguvu ni kwamba nina vigezo vyote so hata wakati naingia haikua ngumu kupata nafasi kwenye shows kubwa. Ndani ya mwaka mmoja nikapata nafasi katika jukwaa kubwa la Swahili Fashion Week.

AFROSWAGGA: Any favourite designers ambao ungependa fanya nao kazi/umeshafanya nao kazi?
JOSH: My favorite designer is Martin Kadinda. Ni mtu ambaye Mungu amempa moyo wa upendo,huruma, heshima na busara na ni msaada mkubwa sana kwa hata wanamitindo wengi nchini.
AFROSWAGGA: Changamoto zozote ulizokutana nazo kazini? Na miaka 5/10 unaionaje tasnia ya uanamitindo? Tutaweza fikia nchi kama Sudan/Nigeria zenye wanamitindo wakubwa duniani?
JOSH: Changamoto zipo nyingi sana lakini ndo tuanaelekea tunashukuru tunaanza kuona support kutoka serikalini… Basata wameanza kua karibu na watu tasnia ya mitindo. Naamini ndani ya miaka miwili ijayo Tanzania itakua miongoni mwa nchi tatu zinazotoa wanamitindo wazuri na ghali zaidi africa. Kwa sasa tuna zaidi ya wanamitindo 5 wanaofanya vizuri nje ya nchi kama vile Flaviana matata, Abel Kipaso, Thomas nguka, Josephine Mumwi pamoja na Zara Bedel
Interview by @willibard_jr
Related posts
5 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More on on that Topic: afroswagga.com/mitindo/pata-kumjua-josh-ipyana-mshindi-wa-master-tanzania-2019/ […]
… [Trackback]
[…] Read More here on that Topic: afroswagga.com/mitindo/pata-kumjua-josh-ipyana-mshindi-wa-master-tanzania-2019/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on that Topic: afroswagga.com/mitindo/pata-kumjua-josh-ipyana-mshindi-wa-master-tanzania-2019/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on to that Topic: afroswagga.com/mitindo/pata-kumjua-josh-ipyana-mshindi-wa-master-tanzania-2019/ […]
… [Trackback]
[…] Read More here on that Topic: afroswagga.com/mitindo/pata-kumjua-josh-ipyana-mshindi-wa-master-tanzania-2019/ […]