Mwanamuziki Barnaba amefunga ndoa na mkewe Raya, wawili hawa walifunga ndoa ya kiislam, walikuwa na sherehe 3 ambapo ni send off ndoa na wakamalizia na reception na tupo hapa kuangalia mavazi ya sherehe zote tatu.
Kwenye ndoa Barnaba alichagua gold and white, ambapo alivaa kanzu nyeupe akamalizia muonekano wake na cream kimono chenye nakshi za gold, belt ya gold aliyo-match na kitambaa kichwani huku Raya yeye akiwa amevalia baby blue look, top na skirt ya blue yenye embellishement za gold akamalizia na mkufu wenye blue na vail yenye blue na gold.


Send off Raya alikuwa na looks mbili ambapo aliingia na hii pink dress na muonekano wa pili ulikuwa ni gold corset, Baranaba yeye alikuwa amevalia two pieces nyeupe zenye nyeusi kwa mbali akamalizia muonekano wake na miwani pamoja na viatu vyeusi.
Tunadhani Barnaba alikuwa simple kumpa Raya nafasi ya ku-shine maana ilikuwa siku yake.


Reception wote walikuwa na looks mbili ambapo waliingia na hii ya kushoto, white mermaid dress yenye urembo chini na huku Barnaba akiwa kwenye blue suit, na look ya pili ilikuwa ni hii white pencil pearled dress huku Barnaba akiwa na purple suit.
Walipendeza tumependa kwamba Barnaba amebana nywele zake vyema, tumependa hakuweka zile wallets zake zinazotunisha mifuko kwenye suruali amekuwa neat.


Well Mavazi yote ya Raya kasoro la siku ya ndoa yanatoka kwa @designed_by_shuu
Nails 💅🏻 @thebossnailstz
Makeup @jodees__makeup / @rosekayuga__
Headpiece @weavefairytz
Hair @sephahair_clinic
Blue Suit Ya Barnaba Inatoka Kwa @mtani_bespoke
Purple Suit Ya Barnaba Inatoka Kwa @sutibega_
Send Off Outfit Ya Barnaba Inatoka Kwa @kanzuland
📸 @chumbachu_ / 📷 @icon_tz
Hongera kwa Maharusi na Tupe Maoni Yako Hapo Chini Look Ipi Umeipenda Zaidi?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…