Watu maarufu mbalimbali walihudhuria katika reception ya mwanamuziki Barnaba na mkewe Raya ambao wamefunga ndoa week iliyopita, well tupo hapa kureview nani alivaa nini na was it giving what it suppose to give au its a failed assignment?
Nandy Na Billnas tunaweza kusema hii ni favorite look yetu of the night, color cordination, fit zimewakaa vyema, stylish, neatly done hair styles & makeup, tumependa kwamba Nandy amevaa nguo ndefu lakini yet ameonyesha some skin kupitia sheer zilizopo pembeni ya gauni. They did that japo kwa Nandy kifuani kidogo ilitaka kuharibu but tunaweza kusamehe.
Suit @jm_international_collection
Dress @nellsoamtee


Wema Sepetu & Whozu, Wema alipendeza na hii yellow dress, tumependa kwamba ameachia nywele lakini mbele zimebanwa vyema kuonyesha makeup na hereni lakini pia kuacha nguo ionekane vyema, the design tumeshaiona mara nyingi kwake we need something new, Whozu alivaa red suit haikuwa mbaya sana kila mmoja akikaa kivyake lakini pamoja imetupa feeling ya vidonge vya amoxicillin all in all wakikaa tofauti tofauti walipendeza.
Suit by @jm_international_collection
Dress by @designed_by_shuu


Hamisa Mobetto alipendeza na gauni yake tunadhanii hii style ya kuvaa gaunifupi then chini ina sheer fabric ndio trend kwasasa, unajua ile unataka kushow off lakini kama hutaki kushow off skin ndio hii, tumependa that ametumia color nyeusi chini imefanya the look kuonekana putted together, makeup na nywele on point.
Dress- @mobettostyles
Mua- @makeupbyjojotz
Hair stylist- @certified_perucaz


Gigy Money alivalia long velvet dress yenye sheer pembeni look ilikuwa nzuri decent hajaonyesha too much skin, lakini ingekua vyema zaidi kama nywele zingenyanyuka since gauni inashingo ndefu kidogo na imefunikwa sehemu nyingi,lakini pia the bag was a miss kwetu.
Hair @luluzhair
Makeup @gigy_money_og
Pochi @vbs_royaltrends
Picha @chizimapicha


Linah Sanga, alivalia short dress ambayo ilikuwa ni off shoulder, idea ya hii dress haikuwa mbaya lakini piece ya juu na chini haviingiliani yaani ni kama vitambaa vilibaki na hawakujua waviweke wapi wakaingizia tu kwenye hii gauni, tunadhani wangetumia fabric moja juu na chini ingependeza zaidi.


Esma Platnumz, tumeona better than this kwa Esma, kwetu tunadhani angeweza kufanya vyema zaidi, vazi tumeshaliona mara nyingi kwa wengine so kuliona kwake ilikuwa afanye zaidi ya wengine lakini imekuwa kawaida, pia viatu alivyovaa na hili vazi haviingiliani, kama unavaa vazi linafika mpaka chini the least unaweza kufanya ni kuvaa open sandals ilikuonyesha skin lakini pia kupata kimo kidogo.Nyele na makeup on point.
Lace @esma_dangote
Fundi @asbahdesign
Makeup @nonoglams
Nywele @certified_perucaz
picha @barty_photographer


Anyways Afromates tupe maoni yako, look ya nani umeipenda zaidi?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…