Zinaitwa tactical bag lakini wengi wanazijua kama vest bag, zimekuwa zikionekana ku-trend kwa sasa ambapo wakati zinaanza zilikuwa zinavaliwa na wanaume tupu lakini muda ulivyozidi kwenda tumekuja kuwaona na wanawake wakiwa wanazivalia as we all know kwa sasa we have a unisex World, tulianza kuwa spot watu maarufu kutoka nje kama Kanye West na Asap Rocky wakiwa wamevalia Vest Bags hizi na zikaongelewa sana kwamba zitakuwa new trend baada ya Fanny Packs
Asap Rocky na Kanye West wao walivaa hii bag kutoka kwa fashion label Alyx, ambapo hii label ilisha wahi kufanya collaboration na Kanye West
Ukiangalia vizuri hii vest bag utagundua nikama fanny pack kasoro hii inamikono miwili so unavaa kama bag pack lakini kwa mbele, ipo in between a vest & a bag.
Well it took zero time before wa kwetu kutoka Tanzania kuziona na kuanza kuzitumia vilivyo kabisa ( kama tunavyojua mapenzi ya wa-Tanzania wengi na trends), tumeona zaidi zikiwa zinavaliwa na group la muziki la WCB kuanzia Diamond Platnumz, Harmonize na Rayvanny
Tumekuwa tukiwaona na hizi vest bags mara nyingi kama hapa ambapo Rayvanny aliivaa wakati ana attend kwenye birthday party ya official dj wa Diamond Platnuzm Romy Jones, yeye alivaa perfectly well our only concern ilikua hakuchoka kuivaa all night long? parting with it feels exhausting na ndio maana huwezi vaa bag pack club au kubeba handbag kubwa lakini waswahili walisema ukitaka uzuri shurti uzurike na mtaka cha uvunguni shurti uiname.
Lakini haikuishia hapo katika label hii ya WCB tukaja kumuona kiungo mwingine kutoka label hio akiwa amevalia hii vest bag yeye aliivaa katika music video ya wimbo alio shirikishwa na prince dully skykes uitwao wa kadamshi, tulishatoa maoni yetu kwa jinsi ambavyo tuli – feel kuhusu mtoko wake huo,ilikuwa too much going on, everything was bold, kuanzia color za outfits, accessories kama hio vest bag na jewerly ilikuwa too much.
Lakini pia mmiliki wa label ya WCB, Diamond Platnumz nae akaona asipitwe na hii trend yeye alivaa wakati ana perform huko Ghana, kama kawaida yake na mapenzi yake kwa sasa yapo katika track pants. Alivaa track pants , kicks za rangi rangi hii tunamuona nayo sana sasa hivi huku akiwa amemaliza na accessories kama vest bag, bandana, tiny glasses na mikufu all we can say kuhusu huu muonekano wa Diamond ni very DISTASTE, mambo yamekuwa mengi hujui upende kipi uchukie kipi and well kwa jinsi ambavyo tumeona watu wakivaa hizi vest bags zinavaliwa kifuani yeye amevaa kwenye tumbo, may be ni trend mpya anajaribu kuiset.
Kama utavaa hii vest bag remember yeyewe ni statement accessory unachotakiwa kufanya ni ku turn down mavazi yako yawe kawaida unless your real good on styling.
Related posts
3 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More on on that Topic: afroswagga.com/mitindo/spotted-diamond-platnumz-rayvanny-harmonize-wakiwa-wamevalia-vest-bag-trend/ […]
… [Trackback]
[…] Info on that Topic: afroswagga.com/mitindo/spotted-diamond-platnumz-rayvanny-harmonize-wakiwa-wamevalia-vest-bag-trend/ […]
… [Trackback]
[…] Info to that Topic: afroswagga.com/mitindo/spotted-diamond-platnumz-rayvanny-harmonize-wakiwa-wamevalia-vest-bag-trend/ […]