Kama kuna kitu tunajua kwa hakika ni kwamba kila mwaka denim (jeans) lazima i-trend na kwa namna za kipekee kabisa, kulikuwa na skin jeans, zikaja mom jeans, tukaenda kwa distressed jeans, kukawa na deconstructed jeans na sasa tumehamia kwenye denim knee high covers.
Denim knee high covers hizi ni kama socks au tight ambazo zinaziba mguu mpaka kwenye goti, hizi haziji na kiatu chake yaani unaweza kuvalia kiatu chochote iwe sandals, boots, raba ni wewe tu na chaguo lako.
Tumeona watu maarufu mbalimbali kutoka Tanzania wakiwa wamevalia trend hii ambapo tumemuona Paula Kajala, Phina na Abby Chams

Well hizi covers zinafaa kuvaliwa usiku, kwenye party na zinaendana sana au kupendeza sana kama utavaa na kitu kingine cha denim juu iwe coat, skirt au pants.
Utaweza kujuliza kwanini nivae?
- Zinakufanya uonekane tofauti (unique)
- Kama unaenda sehemu ina baridi itakukinga na baridi
- Kama kuna mbu na hutaki kuvaa mavazi marefu ina faa pia
- Kama unavaa viatu ambayo hudhani kama vinaendana na vazi ni namna nzuri ya kuficha viatu hivyo
- Kama una insecurity na miguu yako lakini ungependa kuvaa nguo fupi basi ni namna nzuri pia ya kuficha miguu.
Anyways tuambie a clap or slap kwenye hii trend?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…