Aug 22, 2016 Tuliandika hili andiko kuhusu wabunifu, washonaji na stylist nini tofauti zao na jinsi wanavyo fanyakazi zao, karibia miaka miwili imepita tumejaribu kutathimini je kuna maendele yoyote yamefanyaka katika hili swala? stylist wanafanya kazi zao vyema kabisa lakini upande wa wabunifu bado tunachechemea, well leo tumeamua ku throw back na hili andiko labda safari hii wataelewa na kulifanyia kazi
Ime fika muda wa Africa ndani yake tukiwemo wa Tanzania tujue kuna tofauti kubwa mno kati ya mbunifu, stylist na fundi cherehani japo wote wana deal na kitu kimoja mitindo.
Si kila mbunifu ana weza kuwa stylist, si kila fundi cherehani ni mbunifu na si kila stylist ni mbunifu.
tujue kwanza tofauti za watu hawa
Mbunifu huyu ni yule anae chora michoro ya mavazi ana buni vazi liweje kwa kuliweka katika karatasi, huyu ana jua kitambaa gani kitumike, kipi kikae wapi na kipi kikaeje
Fundi cherehani huyu ni baada ya mbunifu kubuni yeye ana pelekewa kushona ile nguo, ana kata makato ya kitambaa na kushona ili ile idea ije iwe reality katika dunia
Stylist huyu yeye baada ya mbunifu na fundi cherehani kufanya kazi zao yeye ana mstyle mtu kwamba nguo hii itanedana ukivalia na kiatu hiki, shati rangi hii na urembo huu. Hawa ni watu watatu tofauti ambao kwa pamoja wana fanya ulimwengu wa mitindo uendelee kuendelea
kilicho tufanya mpaka tuka andika hili ni jinsi ambavyo wasanii wetu wana shindwa kuelewa, week chache zilizo pita kuna baadhi ya wasanii wali tangaza kuwa wana valishwa na baadhi ya watu tulikua na expectations kubwa sana kutoka kwao lakini kuna walio tufurahisha na walio tufanya tuandike hii article leo
Shilole alitangaza kuvalishwa na Kikifashion na Martin Kadinda hawa wote ni wabunifu wakubwa sana Tanzania na tulitegemea callable yao itatoa kitu bora sana lakini imekua tofauti
Shilole/Shishi ame buniwa nguo hatuwezi kusema ni mbaya labda kama kunge kuwa na mkono wa stylist ingekaa vizuri au kuvaliwa vizuri zaidi ya hivi alivyo vaa
Weusi, weusi walitangaza kuvalishwa na cutrite designs ukitembelea instagram yao huto ona sehemu wame andika kama wao ni ma designer, stylist au mafundi cherehani ila kwa kuangalia utajua hawa ni washonaji, wame washonea nguo weusi lakini hawaja wa style wala hawaku buni vizuri
hii ni show ya Fiesta ya nyuma una weza kuona weusi walivaa walikua coordinated as a group, simple ila wame pendeza
hii ni mwaka huu ambapo wame valishwa na mtu binafsi unaweza kuona kuna tofauti kubwa sana hamna uwiano, kila mtu kavaa kivyake rangi haziendani yani its a mess
on the other hand Maua… Maua ame valishwa na the stylist studio.. hawa ni ma stylist pia kuna mbunifu ndani yake ambae ni Rio, Tuna weza kusema Maua me improve alot kutoka alipo kuwa zamani mpaka sasa hata kama nguo zake kime nunuliwa dukani hazija buniwa na the stylist lakini wame mtendea haki Maua, kila kitu kipo on trend na she looked stylish.
Maua kabla ya the stylist
Maua baada ya the stylist
Tuna dhani mme elewa nini tunaongelea kama una maoni una weza kutuachia hapo chini, na pia una weza kutupata katika mitandao ya kijamii
Facebook- afroSwagga
Twitter -Afroswaggatz
Instagram- Afroswagga
Related posts
2 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Info to that Topic: afroswagga.com/mitindo/tofauti-ya-mbunifustylist-na-fundi-cherehani/ […]
… [Trackback]
[…] Here you will find 16827 additional Information to that Topic: afroswagga.com/mitindo/tofauti-ya-mbunifustylist-na-fundi-cherehani/ […]