Ni wazi mitandao ya kijamii imeendeleza kufubaza akili za wabunifu wetu hata kuwafanya kusahau umuhimu wa wao na biashara zao kuwa na website.
Lakini mitandao ya kijamii pamoja na wingi wa watumiaje wake kamwe haitakuja kupoteza umuhimu wa website katika biashara. Ni wazi kupitia mitandao ya kijamii mbunifu anayonafasi kubwa ya kazi zake kuonwa na watu wengi ambao wanatumia mtandao husika, tofauti na website ambapo watu wakaotembelea ukurasa wako ni wale ambao wamedhamiria kweli kuona kile unachokifanya katika biashara yako, ikiwa ni pamoja na bidhaa zako.
Kwa kutumia mfano wa mkongwe Mustafa Hassanali tunaweza kuona tofauti ya website na social media. Picha juu ni muonekano wa website ya Mustafa Hassanali ambayo imepangiliwa vizuri ikiwa na vipengele vinavyoshibisha portifolio yake kama mbunifu. Ukitazama kwa makini utagundua website yake imejikita kwenye kazi yake tu, hii inawasaidia watu ama wateja wake wanapotaka kumfahamu vizuri mustafa, kwa kutembelea website yake tu utagundua yeye ni nani na anafanya nini kwenye tasnia ya mitindo nchini.
Lakini tukirejea kwenye mitandao ya kijamii, utagundua kuwa licha ya kuwa mbunifu mhairi pia anamaisha mengine nje ya jukwaa la mitindo ambayo tunapata kuyafahamu kupitia mitandao yake ya kijamii. Licha ya kuwa huwa anapost baadhi ya kazi zake, lakini hawezi kuweka picha zote, hii inaendelea kumtofautisha Mustafa wa Instagram na Mustafa wa kwenye website yake kibiashara.
Mfano huu mmoja utakupa mwangaza juu ya umuhimu wa wewe kama mbunifu, stylist au model kutotegemea social media peke yake kwenye biashara yako. Ni vema kutumia social media kupeleka wateja kwenye website yako ambapo baadhi ya maswali ambayo watakuwa nayo kuhusiana na kazi zako wataweza kupata majibu yake huko.
Maswali yapo mengi ya kujiuliza, ikiwemo vipi kama wenye mtandao wao wakiamua kuufunga? wakati huo umetumia gharama nyingi kuwekeza kwenye mtandao husika na kujizolea followers wakutosha. Lakini hili haliwezi kutokea ikiwa unawebsite yako. Mtandao ukifungwa bado utakuwa na sehemu ya kuonesha kazi zako.
Sisemi msitumie mitandao ya kijamii kuweka kazi zenu, la hasha…ni vema ukatumia vyote ili kukuza chapa yako na biashara yako kwa ujumla.
Related posts
HOT TOPICS
Happiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/VZ1jH2zJUg
FollowHappiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/689j7Yjcn0
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
Feza Kessy Atuelezea Kuhusu Fashion & Style Zake
Feza Tadei Kessy ni Muimbaji, Muigizaji lakini pia ni mtunzi wa nyimbo lakini pia Fezza ni former beauty queen ambapo mwaka 2005 alikuwa Miss Dar City Centre, Miss Ilala & Miss Tanzania Runner up. Lakini pia alishawahi kuwepo katika Reality Tv Show – Big Brother Africa. Kwa…