Kuna vitu vidogo ambavyo unaweza kupuuzia na kusema havionekani au hata kama vinaonekana sio big deal lakini kiukweli vinaweza kutoa muonekano wako kutoka 100% to 70% kitu ambacho kinakera maana umechukua muda mwingi kufikiria mtoko wako halafu kitu kidogo tu kina uharibu.
- Je unajua vifungo vinaweza kufanya vazi lako lionekane cheap?
Utajiuliza vifungo vinawezaje kufanya vazi lionekane cheap? Kifungo ni kitu ambacho ni rahisi kuwa noticed, vifungo vipo mbele kabisa kama sura hivyo ni rahisi kuonekana kwa haraka.
Namna gani vifungo vinaweza kupunguza hadhi ya vazi lako?
- Kifungo kimeshonwa na uzi rangi tofauti
Unakuta labda kifungo kilichomoka ukaamua kukishona mwenyewe na kwa bahati mbaya hukuwa na uzi unaoendana rangi na vifungo vingine, hii inapunguza u-smart wa vazi lako linaonekana lina dosari hakikisha kama umekosa uzi unaofanana na vifungo vingine basi subiri hadi uupate au shona vifungo vyote kwa rangi ya uzi uliyonayo.
- Kifungo kuwa rangi tofauti na vingine
kama tulivyoongelea kwenye uzi inaweza ikawa kifungo kilichomoka na hukikiona, unakuja kushtuka kimeshapotea unaamua kutafuta kingine chochote unashonea, una haribu show ya vazi lako, kama umeshindwa kupata kinachoendana na vilivyobaki basi shonea vyote kwa vile ambavyo unavyo ili usiweke dosari kwenye vazi lako.
- Vifungo vinavyo ng’aa sana
Umenunua vazi ukakuta vifungo vina scream yaani unaweza kukuta vina rangi fulani inakelele au rangi ni gold lakini ile cheap gold, inasababisha vazi lako kuoneka cheap, badilisha vifungo hivyo na tumia vyenye rangi iliyotulia na inayoendana rangi na vazi lako.
Ni matumaini yetu umejifunza kitu, tuambie ni kosa lipi kati tuliyo yataja umeshawahi ku-commit?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…