Imekuwa kawaida yetu kuchukua muda kutafuta nini kinakwamisha Tasnia ya mitindo Nchini na nini kifanyike ili kuondoa changamoto hizi zinazosababisha kudorora kwa sekta hii mahsusi duniani kote. Mara nyingi tumekuwa tukilalamikia stylists na wabunifu kuhusu kukosa ubunifu na upekee katika kazi zao, wabunifu wanacopy (kunakili) kutoka kwa wabunifu wengine, stylists kadhalika style zao ni zilezile kila siku.
Tumejiuliza swali, je nini kifanyike? Kwanini sisi ni watu wa-kucopy tu? yaani kila unapoona design (mtindo) fulani nzuri basi unakuta kumbe imeibiwa mahala fulani kwa aidha mbunifu mdogo au mashuhuri. Tafakari yetu ikaturudisha nyuma kidogo katika kupembua changamoto hii ambayo imezidi kukuwa katika sanaa ya ubunifu wa mavazi. Katika kutafuta majawabu ya nini hasa kinachangia, Afroswagga ikafanya kautafiti kadogo ambako kamewamulika wateja kama chanzo kikubwa cha kudumaa kwa sanaa hii. Licha ya kuwepo kwa kudumaa kwa ubunifu katika sanaa ya ubunifu, lakini pia wateja wamekuwa na influence (ushawishi) mkubwa katika kuwafanya wabunifu watu washindwe kutoka nje ya comfort zones zao.
Kwa wateja kisanga kinakuja pale mteja anapoenda na mtindo wake kichwani badala ya kumuachia mbunifu kufanya kazi yake. Jamani unapokwenda kwa stylist au mbunifu kutaka service (huduma) unatakiwa umuachie na kumuamini afanye kazi yake. Lakini unapoenda na idea yako hapo huitaji service ya stylist wala mbunifu bali unataka service ya personal shopper na fundi cherehani. Yes personal shopper yeye kazi yake kukununulia mavazi ambayo wewe unayataka wakati stylist yeye kazi yake yeye ni ku-coordinate mavazi ya mteja wake. Na kwa mbunifu kazi yake ni kukubunia vazi wakati fundi cherehani (mshona nguo) yeye kushona ile ambayo imeshabuniwa.
Tunadhani hii inachangia kwa kiasi kikubwa Tasnia yetu kuzorota, inawezekana wabunifu wanajua kubuni na stylist wanajua ku-style lakini hawawezi kwenda kinyume na matakwa ya wateja wao. Tungependa muwaachie wafanye kazi zao, kama umeona kazi yake ukaipenda mpaka ukaamua kumtafuta ni vyema ukamuacha aifanye hio kazi yako kwa namna ambavyo yeye anaweza, hii sio tu itamsaidia mbunifu kuonekana anajua nini anafanya bali pia kukupa wewe muonekano wa tofauti na pia kazi zetu kuonekana kwingine.
Wateja pia huridhika, mfano mara nyingi sisi huwa tunapost wabunifu ambao wamechukua ubunifu kwa mtu mwingine ukisoma comment kwenye post za hizo picha utagundua asilimia kubwa hatuna uelewa wa ubunifu, wengi wanamsifia mbunifu amefanya kazi nzuri kuliko mwenye kazi yake, well yes lazima aifanye vizuri maana kashakuta imeundwa. Yeye anaifanyia marekebisho machache anaiachia huko nje. Tunasahau yule ambae alituliza kichwa chake akabuni kuanzia chini.
Pale ambapo mteja anapo sema ni sawa mbunifu ku-copy mbunifu mwingine sababu hamna cha ajabu vyote vimesha fanywa inatufanya tuwaze, “inakuaje wabunifu wa wenzetu wanafanya kazi zinatoka zikiwa zina extra touch’s halafu sisi tunasema vyote vilisha fanywa?” Ni kweli skirt haiwezi kubadilika itaitwa skirt au gauni lakini ni nini unaongezea katika hilo vazi ndicho kinacho matter na kuitwa ubunifu.
Licha ya wateja kuwa chanzo cha kucopy kwa kazi za watu, lakini mwarobaini wa tatizo hili ni pale tu mbunifu atakapo anza kutoa collection zake mwenyewe ambazo ni kwa ajili ya kuonesha wateja uwezo wake. Tunajua changamoto ya wabunifu wengi kushindwa kutengeneza collections zao ambazo zimekuwa zimebuniwa kwa ajili ya kushowcase ni mtaji, lakini taratibu tutafika. Sio lazima uanze na collection ya nguo 10 au 20. Anza na ulichonacho, waache wateja waone uwezo wako jinsi unavyoweza kubuni na kudesign mtindo mbalimbali ambayo wanaweza kuvaa.
Related posts
5 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Here you can find 92701 additional Info to that Topic: afroswagga.com/mitindo/wateja-wanachangia-kudumisha-sekta-ya-mitindo-nchini/ […]
… [Trackback]
[…] There you will find 51214 additional Information on that Topic: afroswagga.com/mitindo/wateja-wanachangia-kudumisha-sekta-ya-mitindo-nchini/ […]
… [Trackback]
[…] There you will find 74338 more Info to that Topic: afroswagga.com/mitindo/wateja-wanachangia-kudumisha-sekta-ya-mitindo-nchini/ […]
… [Trackback]
[…] Find More here on that Topic: afroswagga.com/mitindo/wateja-wanachangia-kudumisha-sekta-ya-mitindo-nchini/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on to that Topic: afroswagga.com/mitindo/wateja-wanachangia-kudumisha-sekta-ya-mitindo-nchini/ […]