Stretch Marks (michirizi) hutokea sehemu mbali mbali za mwili, mikononi, miguuni, mapajani, tumboni nk, wengi hutokewa kutokana na kuongezeka kwa mwili (kunenepa) au Ujauzito hii hutokana na ngozi kutanuka. Wengi hawaipendi na wana tafuta namna ya kuziondoa unaweza kuondoa stretch marks naturally (kwa njia za asili) bila kwenda kununua madawa ya bei ghali.
1) MAFUTA YA MNYONYO
Mafuta ya mnyonyo husaidia sana kwenye ngozi kama mikunjo ya ngozi husoni, chunusi, mabaka meusi kwenye ngozi lakini pia husaidia katika kuondoa michirizi.
- paka mafuta ya mnyonyo mahala palipo kuwa na michirizi
- funga eneo hilo kwa mfuko wa plastic kama uonavyo pichani
- kisha weka kitu chenye joto juu ya mfuko huo kama heating pad au chupa ya maji ya moto kwa dakika ishirini (20) kila siku mpaka utakapo ona mabadiliko.
2)ALOE VERA husifika kwa kutibu magonjwa mbali mbali ya ngozi hivyo pia husaidia kuondoa michirizi hii ya ngozi kwa njia mbili zifuatazo,
- kwanza unaweza kupaka Aloe Vera tu na kuiacha ikae kwenye sehemu iliyo kuwa na michirizi kwa dakika 15 kisha uoshe kwa maji ya vuguvugu au,
- njia ya pili, ni kuchanganya majimaji ya Vitamin A, Vitamin E na Aloe Vera yenyewe kisha paka kwenye eneo lililo athirika na michirizi kila siku. Paka kama mafuta ya kupakaa mwilini.
3)SUKARI
- Chukua sukari mbichi kijiko kimoja, mafuta ya Almond na Maji maji ya ndimu, changanya kwa pamoja halafu paka pale palipo athirika
- Fanya hivi kila siku kabla ya kwenda kuoga, fanya kwa mwezi mzima na utaona matokeo yake.
4) JUISI YA VIAZI vina vitamini na madini ambayo kukuza ukuaji wa seli za ngozi.
- kata kata kiazi chako katika vipande vyembamba
- chukua kipande cha kiazi na ukisugue pale kwenye michirizi yako hakikisha yale maji ya viazi yame ingia kwenye michirizi ako.
- kaa nayo kwa muda na kisha uondoe kwa maji ya uvugu vugu.
Related posts
3 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More on that Topic: afroswagga.com/skin-care/njia-za-kuondoa-michirizi-stretch-marks/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on that Topic: afroswagga.com/skin-care/njia-za-kuondoa-michirizi-stretch-marks/ […]
… [Trackback]
[…] There you will find 41042 more Information to that Topic: afroswagga.com/skin-care/njia-za-kuondoa-michirizi-stretch-marks/ […]