Mahitaji:
viazi mviringo/mbatata – kg1
unga wa ngano – 1/2kg (nusu kilo)
binzar (rangi ya mchuzi) – kijiko kimoja
malimao au ndimu – 4
chumvi kiasi
maji ya kutosha kulingana na mahitaji
kidokezo:Unaweza kuongeza vitu vya ziada kama nyama au mboga mboga kulingana na mahitaji yako
Mandaalizi:
- Safisha viazi mbatata/ mviringo bila kumenya kisha vichemshe, chemsha hivyohivyo bila kumenya hakikisha havivurugiki vikiiva ipua na uviweke pembeni,
- Bandika sufuria lingine la maji huku pembeni ukikoroga unga wa ngano uliochanganywa na maji (uji wa ngano) kwenye bakuli, endelea kukoroga unga wa ngano mpaka uwe mwepesi na usiwe na madonge, kisha weka binzari.
- Maji ya jikoni yakishachemka, mimina mchanganyiko wako wa ngano na binzari kwenye maji ya moto koroga uji wako hadi ushike vizuri uji ukisha shika vizuri kamulia malimao na punguza moto na uuache uji uendelee kuchemka, wakati uji ukiendelea kuchemka menya vile viazi vyako ulivyo vichemsha mwanzo na uvikate vipande saizi ya kati kisha vimimine (tumbukiza) katika uji uliopo jikoni. acha mchanganyiko wako uchemke kwa dakika tano kisha ipua urojo wako utakuwa tayari kuliwa.
KIDOKEZO: Unaweza kuchanganya urojo wako na kachori, bagia, mishikaki, crips za viazi au mihogo iliyo katwa katwa vipande vidogo vidogo PIA unaweza weka mboga mboga (figiri, majani ya kitunguu maji,kabichi) tayari kwa kuliwa.
Related posts
5 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More Information here on that Topic: afroswagga.com/uncategorized/jinsi-ya-kuandaa-uji-wa-urojo/ […]
… [Trackback]
[…] Information on that Topic: afroswagga.com/uncategorized/jinsi-ya-kuandaa-uji-wa-urojo/ […]
… [Trackback]
[…] Here you can find 37886 additional Information to that Topic: afroswagga.com/uncategorized/jinsi-ya-kuandaa-uji-wa-urojo/ […]
… [Trackback]
[…] Find More Information here on that Topic: afroswagga.com/uncategorized/jinsi-ya-kuandaa-uji-wa-urojo/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Info here to that Topic: afroswagga.com/uncategorized/jinsi-ya-kuandaa-uji-wa-urojo/ […]