MAANDAZI
Vipimo
Unga – 5 Vikombe
Tui la Nazi zito vugu vugu – 1 ¼ kikombe
Sukari – 3/4 kikombe cha chai
Samli iliyoyayushwa au mafuta – 3 vijiko vya Supu
Hamirah – 2 Vijiko vya Supu
Hiliki – 1/2 Kijiko cha chai
Mafuta ya kukaangia
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
- Ndani ya kibakuli kidogo, mimina hamira na na vijiko viwili vya kulia vya tui. Weka kando mpaka hamira ianze kufura, kama dakika 5-10.
- Pasha samli moto
- Ndani ya bakuli kubwa au sinia, changanya unga, sukari, iliki na samli ikiwa bado moto moto.
- Mimina hamira ndani ya mchanganyiko wa unga. Changanya na ukande huku ukitumia lile tui la nazi. Tui likipungua unaweza ukaongeza maziwa. Kanda unga mpaka uwe laini.
- Kata madonge *12 au 15 uyaweke kwenye baraza iliyonyunyiziwa unga na uyafunike ili yapate kufura na yasikauke.
- Madonge yakifura, sukuma kama chapati kisha ukate mara nne kama kwenye picha. Endelea kufanya hivyo na madonge yote. Yawache maandazi yafure tena baada ya kukata kama dakika 15 hivi.
*Ukipenda maandazi manene fanya madonge 12. Ukipenda mepesi fanya madonge 15
- Pasha mafuta moto kwenye karai. Maandazi yako tayari kukaangwa sasa.
- Kaanga maandazi kwenye mafuta ya moto. Upande mmoja ukifura na kuwa rangi nzuri geuza upande wa pili. Endelea nama hii mpaka maandazi yote yawe tayari.
Vidokezo: Kuhifadhi Maandazi
- Unaweza kuweka unga wa maandazi uliyokwisha kuyakata ndani ya freezer
yakisha umukua ikiwa unataka kutumia siku nyengine. Tumia waxed paper na unga wa kutosha kuweka katikati ya maandazi ili yasishikane unapoya freeze kwanza katika freezer. Yakishika barafu, toa na yafunike kwa wax paper kiasi kama matano pamoja na uyatie katika freezer bags. Ukitaka kukaanga maandazi siku nyengine, toa maandazi mapema kidogo yatoke barafu kidogo tu. Pasha mafuta moto kwenye karai na kanga maandazi.
- Vile vile unaweza kuyapika kabisa na kuweka katika freezer bags, ukitaka kutumia ni kuyatoa tu na kupasha moto katika Microwave.
MBAAZI ZA NAZI
Vipimo
Mbaazi za kopo (pigeon peas) -40 fl oz (vikopo viwili) (Vikombe vitatu)
Ikiwa mbaazi kavu – 3 Vikombe
Tui la nazi zito – 1 Kikombe
Kitunguu – 1
Chumvi kiasi
Pilipili mbichi- 2
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
- Ikiwa ni mbaazi kavu, roweka katika maji kwa muda wa masaa kisha chemsha hadi ziwive.
- Ikiwa ni mbaazi za kopo, mwaga maji yake ya kopo umimine katika sufuria.
- Kata vitunguu na utie katika mbaazi.
- Tia tui, chumvi, pililipili mbichi upike hadi kwa muda mdogo tu hadi tui lipunguke kidogo, zitakuwa tayari kuliwa.
Related posts
4 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More Information here to that Topic: afroswagga.com/uncategorized/mbaazi-kwa-maandazi/ […]
… [Trackback]
[…] Information on that Topic: afroswagga.com/uncategorized/mbaazi-kwa-maandazi/ […]
… [Trackback]
[…] Read More here on that Topic: afroswagga.com/uncategorized/mbaazi-kwa-maandazi/ […]
… [Trackback]
[…] Info to that Topic: afroswagga.com/uncategorized/mbaazi-kwa-maandazi/ […]