SAMBUSA ZA KUFUKIZA
Mahitaji:-Manda za sambusa za tayari, 20-30
Nyama ya kima nusu kilo
Mchanganyiko wa thomo na tangawizi mbichi vijiko 3 vidogo
Mchanganyiko wa bizari kijiko 1 kikubwa
Kitunguumaji kimoja kikate udogo
Dania moja ikate udogo
Maji ya limau moja
Chumvi kiasi
Na mafuta ya kukaangia baadae lita mojaNA KATIKA KUUNGANISHA SAMBUSA HIZO UTAHITAJI:-
-Unga wa ngano kikombe kasorobo
-na maji kiasi.JINSI YA KUANDAA:-
Ipike nyama yako kwanza ya kima kwa kuichapua kwa michanganyiko ya thomo na bizari, imwagilie maji ya limau, vitunguumaji na dania kiasi…
Ipike nyama hiyo moto wa chini kwa kuikoroga koroga kwa mwiko ili iachane na kuwa moja moja, kusudio likiwa kuipa sura nzuri na iwe rahisi kwako kufunga kwenye manda…
Ipike nyama hiyo hadi iashirie kukauka, bila ya kusahau chumvi kiasi…
Iwache ipoe kiasi ya kuunda gundi ya kufungia manda hizo…
Changanya huo unga na maji kwenye kibakuli hadi upate mchanganyiko mzito…
Sasa kufukiza kwenyewe kunakuja hivi..:-
Katika ganda la kitunguu, teua kile kiganda cha ndani, unda kama shimo kwenye sufuria ya nyama na weka hilo ganda,lipakie mafuta kidogo kisha chukuwa kikaa cha moto, kibwage kwenye hilo ganda na mafuta..huo moshi ndio mpango wote..finika hiyo sufuria kwa muda wa robo saa ili moshi utapakae na kuipa nyama yako harufu kama nyama choma…
Baada ya hapo funga sambusa zako kwa kutumia manda na tayari kuzikaanga…
Bandika karai motoni, mimina mafuta na yakianza kushika moto zikaange kwa makini…
Ukitaka kufaidi rangi nzuri sawia kwa upishi huu, moto uwe wa chini na usichome sambusa yakiwa mafuta moto sana
Mahitaji:-
Maziwa nusu litre
Tende habba 7 hadi 11 zilizotolewa konde
Na vidonge vya barafu iwapo utahitaji.
Jinsi ya kuandaa:-
Kwa tende ulozitoa kokwa, ziweke kwenye bakuli safi kwanza …
Kisha tumia maji moto kiasi na umimine juu ya hizo tende, wacha zikae hivyo kwa nusu saa…
Kisha mwaga maji na bakisha tende pekee…
Baadae Kwenye blender, mimina maziwa yote kisha umimine na tende, saga hadi huo mchanganyiko uwe rojo rojo…
Mimina kwenye jagi na waweza zizimua kwa vidonge vya barafu au ukanywa hivyo ilivyo.
Related posts
4 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More here on that Topic: afroswagga.com/uncategorized/sambusa-na-maziwa-ya-tende/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on to that Topic: afroswagga.com/uncategorized/sambusa-na-maziwa-ya-tende/ […]
… [Trackback]
[…] Information to that Topic: afroswagga.com/uncategorized/sambusa-na-maziwa-ya-tende/ […]
… [Trackback]
[…] Here you will find 29259 more Information on that Topic: afroswagga.com/uncategorized/sambusa-na-maziwa-ya-tende/ […]