Vitumbua
Mahitaji na vipimo
- mchele kilo 1
- nazi kubwa 2
- hiliki kiasi
- sukari robo kilo
- hamira kiasi kijiko kimoja nusu ( itategemea aina ya hamira)
- mafuta nusu lita
- mayai 3 (ukipenda)
namna ya kupika
- uroweke mchele uliokwisha uchambua vizuri na kuupeta.
- utandaze sehemu safi ukauke, kisha usage upate unga mlaini
- kuna nazi uchuje tui zito
- saga hiliki, changanya na sukari
- changanya ule unga wa mchele, sukari, hiliki, tui la nazi na hamira. uvuruge uwe mwepesi kiasi cha kuweza kuchoteka kwa upawa. Acha uumue kwa dakika 25 hadi 30 kutegeme na ubora wa hamira.
- weka kikaango cha kukaangia vitumbua jikoni, anza kukaanga vitumbua vyako kwa kueka mafuta kwanza yapate moto, kisha unachota kwa upawa unga na kueka kwenye vijungu vya kikaangio chetu. unaacha vichemke upande mmoja, kisha unageuza upande wa pili, vikishaiva vitoe weka kwenye chujio ili mafuta yajichuje. Endelea kukaanga viliobakia mpaka unga uishe
vitumbua hivi vinaweza kuliwa na chai, maziwa, uji na hata juice ukipenda na mchuzi.
MCHUZI WA KAMBA
Vipimo
Viazi (mbatata) – 2
Kamba – 1 Lb
Vitunguu – 2
Nyanya – 2
Pilipili hoho – 1
Kitunguu saumu – 1 kijiko cha chai
Tangawizi – 1 kijiko cha chai
Uzile (bizari ya pilau ya unga-Jiyra) – ½ kijiko cha chai
Pilipili manga – ½ kijiko cha chai
Pilipili ya unga – ½ kijiko cha chai
Nyanya ya kopo – ½ kijiko cha chai
Chumvi – kiasi
Namna Ya Kutayarisha
1) Changanya kamba na thomu, tangawizi, pilipili manga, pilipili ya unga, jira na chumvi.
2) Katakata vitunguu weka pembeni.
3) Katakata pilipili hoho weka pembeni.
4) Katakata Nyanya weka pembeni.
5) Menya viazi na uvikate vidogo vidogo.
Namna Ya Kupika
1) Kaanga kamba mpaka wabadilike rangi, watie kwenye bakuli.
2) Kaanga viazi mpaka viwive na vibadilike rangi, vitoe, mimina kwenye bakuli.
3) Kaanga pilipili hoho viwive na vibadilike rangi, vitoe.
4) Kaanga vitunguu mpaka vibadilike rangi, mimina nyaya kaanga pamoja, kisha tia nyanya ya kopo na chumvi
5) Endelea kukoroga.
6) Mimina maji kama robo kikombe, ukishawiva vizuri, mimina katika bakuli la mchanganyiko na ukoroge kidogo ili vichanganyike tayari kwa kuliwa.
Related posts
5 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More on to that Topic: afroswagga.com/uncategorized/vitumbua-kwa-mchuzi-wa-kamba/ […]
… [Trackback]
[…] Read More to that Topic: afroswagga.com/uncategorized/vitumbua-kwa-mchuzi-wa-kamba/ […]
… [Trackback]
[…] Find More here to that Topic: afroswagga.com/uncategorized/vitumbua-kwa-mchuzi-wa-kamba/ […]
… [Trackback]
[…] Read More here on that Topic: afroswagga.com/uncategorized/vitumbua-kwa-mchuzi-wa-kamba/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on that Topic: afroswagga.com/uncategorized/vitumbua-kwa-mchuzi-wa-kamba/ […]