Hakuna kitu kinaudhi au kukera wengine kama uchafu, iwe kinywa, makwapa au hata mazingira machafu yanakera. Inawezekana pia una jitahidi sana kujisafisha lakini hufikii lengo unalolitaka leo tunakuletea Tips ambazo zinaweza kukusaidia ku-level up hygienne game yako.
Sugua Makwapa Mara Mbili
Kama ambavyo inashauriwa ukiwa unaosha uso u-double cleanse basi kuoga napo ni hivyohivyo, hakikisha unaoga mara ya kwanza na sabuni kisha rudia tena, hakikisha unasugua makwapa mara mbili ili mara ya kwanza ni kuondoa zile layers za perfume na jasho na mara ya pili ni kulisafisha zaidi,
Note: unaweza kutumia sabuni ya kipande mara ya kwanza na mara ya pili ukatumia body wash au ukatumia sabuni inayo nukia hii itakupa harufu nzuri mwilini
Piga Mswaki Mara Mbili Kwa Siku
Kama unaoga asubuhi na jioni basi piga mswaki mara mbili pia asubuhi na jioni, kama unatatizo la kunuka kinywa basi itakusaidia kupunguza tatizo hilo kwa kiasi kikubwa lakini pia hata kama huna tatizo hili ni vyema ukapia mswaki mara mbili ili kuweka hali ya kinywa chako sawa.

Osha Nywele Weekly / Kila Baada Ya Week Mbili
Nywele nazo hunuka unaweza ukaoga vyema, ukapiga mswaki vyema lakini bado ukajishtukia una kiharufu personal kumbe ni nywele, iwe ni nywele asilia, rasta, wig au weaving hakikisha unazisafisha kila week na ikishindikana basi mara mbili kwa week hii itakusaidia kuwa smart.
Badilisha Mavazi ya Ndani Daily
Tunajua boxer na chupi mnajitahidi kubasilisha tatizo ni hizo vest na sidiria, hizo nazo zinashika uchafu perfume juu ya perfume na majasho ya kila siku lazima zitavunda, jaribuni kubadilisha mara kwa mara hata kama sio kila siku basi hata kila baada ya siku mbili.
Tutakuja na mengine lakini tumabie pia ni nini huwa unafanya kuwa fresh siku zote?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…