Weekend ni ule muda wa kujijali (selfcare) na ni kawaida yetu kukumbuka kujifanyia usafi sehemu mbalimbali za miili ikiwa ni kutengeneza nywele, kucha, skin care, kufua mavazi etc. Lakini kuna sehemu kadhaa za mwili huwa tunasahau kusafisha na tupo hapa kukumbusha sehemu hizo na kwanini uzifanyie usafi weekend hii.
- Kitovu
Wengi huwa tunasahau kusafisha kitovu kwa namna moja au nyingine ni sehemu ambayo haionekani hasa weekdays tunavaa mavazi marefu kinafichika lakini imagine weekend unataka kwenda out uvae crop top halafu kitovu kichafu, girl makeup popi’n, una wig ya maana, dress code on point then mtu anaangalia kitovu kichafu (shame). Lakini ukiachana na hayo hata kama huvai crops unaweza kusababisha bacteria na tunajua kitovu ni sehemu sensitive, kisafishe leo.
Chini Ya Maziwa
Hii ni sehemu nyingine ambayo wengi huwa tunasahau kusafisha, kwakuwa na yenyewe haionekani basi huwa hatuichukulii maanani, lakini ni vyema ukasafisha vizuri chini ya maziwa na kupakausha vizuri pia unaweza kupata fungus kama hupakaushi au kupaacha pachafu.
Masikio
Iwe nyuma ya masikio,ndani ya masikio au kwenye vitundu vya masikio hakikisha una safisha sikio zima, haileti picha nzuri kuwa na sikio chafu na kwenye matundu ya sikio mara nyingi huwa panatoa harufu kama hapasafishwi, unakutana na watu wanakuhug wanaondoka na harufu, please pasafishe this weekend.
Nyuma Ya Shingo / Magoti
Unavaa zako short skirt/pant na off shoulder top lakini huku nyuma magotini na mgongoni kunaonekana kuchafu haileti picha nzuri unaonekana unavaa vyema lakini hujui kujisafisha hakikisha umesugua ondoa uchafu wote na paka mafuta.
Well tuambie hapo chini ni sehemu gani nyingine muhimu kufafisha?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…