Ukiachana na kuwa dawa nzuri ya kutuliza maumivu, aspirin ina sifika kwa kuwa ni tiba nzuri ya ngozi. Vidonge hivi vinavyo sifika katika kutuliza homa, kichwa au maumivu yoyote pia ina sifika kuwa ni tiba ya ngozi. Kama utakuwa una tumia dawa hizi mara kwa mara katika urembo una weza kupata ngozi yenye afya na nyororo, hii ni kwa sababu aspirin ina acid itwayo acetylsalicylic ambayo husaidia kutibu sehemu iliyoathirika, japo kuwa na sifa hizo lakini pia ina hitajika kuwa muangalifu wakati wa matumizi, kizuri kuhusu aspirin ni kwamba mtu mwenye ngozi ya aina yoyote ana weza kutumia
Aspirin kwa sensitive skin
- vidonge vinne vya aspirin
- plain yogurt (mtindi) vijiko viwili
pondaponda aspirin zako mpaka upate ule unga unga kisha changanya na vijiko viwili vya mtindi, paka katika uso wako na uache ikae kwa dakika 15, kisha futa mask hio kwa kutumia kitambaa chenye unyevu, aspirin husaidia kufungua vitundu vilivyo zibwa wakati mtindi una mosturize ngozi yako. mchanganyo wa vitu hivi una weza kusaidia ngozi yako na kuing’aza
Aspirin na limao kwa ajili ya kusafishia ngozi
- vidonge vinne vya aspirin
- vijiko viwili vya limao
weka vijiko viwili vya juice ya limao kisha ingiza vidonge vya aspirin vyote, vichanganye mpaka viyeyuke kisha paka usoni kaa nayo kwa muda wa dakika 10 na osha kwa maji masafi. Hii husaidia kusafisha ngozi na huondoa madoa.
Aspirin kwa ajili ya kutibu chunusi
- vidonge vitatu vya aspirin
- asali kijiko kimoja
- maji kijiko kimoja
changanya maji na aspirin mpaka vidonge viyeyuke kisha ongezea kijiko kimoja cha asali, paka usoni kwa dakika 10, kisha ufute baada ya kufanya hivi utaona black heads na wahite heads zilizo kuwepo usoni zimekauka.
aspirin facial mask kwa ajili ya kung’aza ngozi
- aspirin vidonge vitatu
- apple cider vinegar kijiko kimoja
- maji vijiko vinne
dillute vidonge vyako na maji mpaka vitakapo yeyuka, ongezea apple sider vinegar na paka usoni, kaa nayo dakika 10 kisha ondoa utapata ngozi nga’vu
aspirin kwa ajili ya ngozi yenye mafuta
- aspirin – vidonge vitatu
- maji – kijiko kimoja
- tea tree oil -3-4 drops
saga aspirin zako mpaka upate unga unga kisha changanya maji na tea tree oil pamoja na unga wa aspirin, paka na ufute/osha uso baada ya dakika 20
aspirin kwa ajili ya ngozi kavu
- aspirin – vidonge vitano
- asali -kijiko kimoja
- almond oil – 3 mpaka 4 drops
- maji – kijiko kimoja
saga aspirin zako mapak upate unga unga, weka maji, asali na almond oil, paka mchanganyiko wako usoni kwa dakika 20, kisha nawa uso kwa maji ya vuguvugu
kama utajaribu husisite kutuandikia matokeo kupitia
Instagram – afroswagga
Facebook – afroswaggamag
Twitter – afroswaggatz
Related posts
HOT TOPICS
We need to have some sort of bima ila for enjoyment. Yaani wanakata ka % ka mshahara kako unakua na card ukienda se… https://t.co/W9oDoaN2YY
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…