Kuna ule msemo unasema face card never decline, week hii tumeona watu maarufu wengi wakiwa kwenye mionekano mizuri ambapo wengi wame serve face na makeup zao pamoja na hair styles za kuvutia
Ambacho kinatuvutia kwasasa ni kwamba watu wengi maarufu wamejua umuhimu wa makeup na nywele nzuri kwenye mionekano yao, tunapenda kwamba wanatilia mkazo kwenye hivi vitu.
Leo tupo na wachache ambao tumewaona week iliyopita tukavutiwa na looks zao akiwepo Mwamvita Makamba akiwa kwenye professional photoshoot, ameachia nywele zake akiwa na makeup ambayo ni suitable kwaajili ya professional look, mwingine ambae tumemuona ni Monalisa yeye alikuwa na birthday amefanya photoshoot akiwa ameachia nywele zake vyema na simple makuep look, Rosa Ree a.k.a mama Omoll alikuwa na bob hairstyle akamaliza muonekano wake na bold red lipstick

Lakini kuna ambao wametuonyesha huitaji nywele ndefu kupendeza na makeup yako, unaweza kuwa na nywele fupi na ukapaka makeup vizuri ukapendeza akiwepo mwanadada Feza Kessy akiwa kwenye blonde low cut akiwa anasheherekea siku yake ya kuzaliwa Fezza alichagua simple neat makeup, Jojo Gray kama wedding guest ametuonyesha namna unaweza kurock low cut harusini, akiwa na low black haircut amemalizia muonekano wake na nude makeup huku mwanamitindo jasinta yeye nae akiwa na blonde low cut ametuonyesha unaweza kuwa na a no makeup makeup look na ukapendeza kwenye mizunguko yako ya kawaida

Tuambie muonekano wa nani umependezwa nao zaidi?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…