Inawezekana unajua na inawezekana haujui kama unachofanya ni dhambi katika ngozi yako na unatakiwa uache kukifanya kwasababu inaweza kuwa ni sababu ya ngozi yako kuharibika
- Kukaa Sana Juani Bila Ya Kupaka Sun Screen
sunscreen ni nini? Sun screen ni lotion au cream ambayo imetengenezwa kulinda ngozi na jua, na sio tu ukiwa juani bali inashauriwa kupakwa hata kama haupo juani, Inafaida nyingi ikiwepo Kutokupata mikunyanzi ya uzee, kuondoa / kutopata madoa usoni lakini pia kukuepusha na maradhi ya cancer
Umuhimu Wa Kupaka Sunscreen Katika Ngozi
- Kutokunywa Maji Ya Kutosha
Maji yanafaida mbali mbali katika ngozi na ni moja ya dawa kubwa ya kuwa na ngozi nzuri na yenye afya hufanya ngozi kung’aa kwa kuwa na afya, pia kupungua/ kumaliza chunusi maana viwango vya maji na mafuta kwenye ngozi vinakuwa katika uwiano. Hydration is the key inashauriwa kunywa litre mbili za maji kwa siku. Hii sio tu inasaidia kwenye ngozi lakini pia katika afya ya mwili wako
- Kuosha Uso Haraka
Wote huwa tumechoka hasa wakati wa usiku umesha choka na kazi yet unatakiwa ufanye skin care routine ya usiku basi unanawa tu harakaharaka umalize upate kupumzika, hii ni dhambi kwa maana unaweza ukanawa na uso ukawa haujasafishika. Chukua muda wako kuuosha taratibu na pitisha sabuni kila mahali, hakikisha unaosha uso wako si chini ya mara mbili lakini pia usizidishe.

- Kupata Ushauri Wa Vipodozi Kupitia Rafiki Yako
Katika vitu ambavyo vinatu-cost wengi ni kuuliza kwa marafiki utumie kipodozi gani, au kwa sababu ngozi ya rafiki yako nzuri unamuuliza anapaka nini na wewe ukapake, hii ni dhambi kubwa ya ngozi. Kwa sababu wote hatuna ngozi sawa kinachomfaa yeye kinaweza kisikufae wewe na kinaweza kuharibu kabisa ngozi yako. Hakikisha unaenda kwa wataalamu wa ngozi kwa ushauri bora
- Kutokusafisha Vifaa Vyako
chochote ambacho kinagusa ngozi yako ya uso kinatakiwa kisafishwe mara kwa mara, kama simu, makeup brushes, taulo, mashuka pamoja na foronya zake. Kwenye hivi vitu kunaweka kuwa na dead skin cells na bacteria zilizo jitengeneza, lakini sio tu hivyo mikono yetu nayo inatakiwa kuoshwa mara kwa mara ikiwa tunagusa na kushika vitu mbalimbali kisha tunashika nyuso zetu bila kujua inaweza kutuletea madhara.
Sababu 3 Muhimu Za Kwanini Usafishe Makeup Brushes Zako
Afromates tuambie wewe ni dhambi gani una commit mara kwa mara lakini pia kuna muendelezo utakao kuja hivi karibuni
Related posts
3 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Info to that Topic: afroswagga.com/urembo/dhambi-za-ngozi-unazotakiwa-kuziacha/ […]
… [Trackback]
[…] There you can find 81413 more Information on that Topic: afroswagga.com/urembo/dhambi-za-ngozi-unazotakiwa-kuziacha/ […]
… [Trackback]
[…] There you will find 63320 more Information to that Topic: afroswagga.com/urembo/dhambi-za-ngozi-unazotakiwa-kuziacha/ […]