Perfume can be the cherry on top when it comes to represent ourselves hii ni kama itatumika vyema lakini kama itatumika vibaya unaweza kuwa labelled kama perfume offender, sote tunapenda kunukia vyema popote tulipo lakini kuna sehemu zinafaa kuwa na perfume za aina fulani mfano mzuri ni kazini / ofisini.
- Je Perfume Zinaruhusiwa Kazini
Inategemea na sehemu unayofanya kazi kuna ambao wanaruhusu na ambao hawaruhusu kutokana na sababu mbalimbali, na perfume hupakwa kutokana na sehemu unayofanya kazi mfano kama unafanya kazi kwenye vituo vya afya mara nyingi unashauriwa kutokutumia manukato, kama ni office /retail inashauriwa kutumia manukato sahihi na kama ni kazi za nje basi hapa mara nyingi unaweza kutumia manukato yoyote.
Kazi yoyote ambayo utakuwa unafanya ni vyema ukajua nguvu ya perfume kwa mazingira yanayo kuzunguka, hizi ni tips chache za nini ufanye na nini usifanye kutumia manukato ofisini,
- Chagua Manukato Yasiyo Nukia Sana
Unapokuwa ofisini hakikisha unatumia light scents, wenyewe tunaita harufu za kizungu hakikisha unanukia lakini sio mpaka unawakera wengine, manukato yako yawe ambayo yananukia kiasi.
Aina Na Namna Ya Kuchagua Perfume Inayo Kufaa
- Less Is More
Unapokuwa ofisini hakikisha unapulizia manukato yako kwa kiasi,na ili yadumu muda mrefu basi pulizia zile sehemu ambazo zinafanya manukato yakae muda mrefu kama shingoni, nyuma ya masikio na kwenye wrist (kiganja)
Sehemu Za Kupuliza Unyunyu “perfume” Idumu Kwa Muda Mrefu
- Wafikirie Wengine
since ofisini kuna watu wengi na unakaa masaa mengi zaidi ni vyema ukawafikiria na wengine, kuna ambao wana allergies au wako sensitive na manukato unaweza kuwa unawaumiza au kuwakera basi hakikisha unapaka manukato ambayo yatakuwa sawa na wengine.
- Usipake Au Ku-Reapply Perfume Ofisini
Uko ofisini na wengine unatoa perfume yako kwenye pochi unaanza kujipulizia au imefika mida ya mchana unaenda chooni una-reapply perfume hii ni nzuri kama una perfume ambayo hainukii sana ila kama inatumia muda kupoa then hakikisha ukijipulizia asubuhi imetosha usiende kukera wengine tena.
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…