Umeshawahi kuanza kupaka kipodozi kisha ngozi yako ikaharibika zaidi ya ilivyokuwa mwanzo? Yes hii huwa inatokea na mara nyingi wengi wetu huwa tunachukulia hii kama dalili ya kipodozi kutokutupenda au ku-fail.
Leo tunakuletea au kukufahamisha juu ya Skin Purging, Skin Purging hii ni pale unapoanza kutumia product mpya za ngozi na ukaanza kuona ngozi yako inazidi kuharibika, hii ni process ya ngozi kusafishwa ambapo ngozi inajiondoa yenyewe ya mafuta, bakteria, au uchafu na ndipo unapoona chunusi zinatokea kuliko kawaida lakini kitu kizuri juu ya Skin Purging ni kwamba haikai muda mrefu huchukua week chache na zinapotea.
Lakini pia haimaanishi kila mtu ataona skin purging, hii hali hutegemea na ngozi ya mtu wengine zinaweza kusafishika tu bila ya kuharibika wakati wengine wanapitia skin purging na pia inategemea na ukubwa wa tatizo lako ndani ya ngozi ambacho kinatakiwa kutolewa nje ili kupata ile ngozi unayoitaka.

Jambo lingine la kuzingatia: Wakati wa utakaso (Skin Purging) baada ya kuanza utaratibu mpya wa kutunza ngozi au baada ya kutumia vipodozi vipya, chunusi ambazo ni ndogo huwa hazionekani kwa jicho la kawaida zinaanza kutoka chini na kuja juu ya ngozi sehemu ambazo uhathirika zaidi na skin purging ni kwenye paji la uso, kidevu pamoja na sehemu za puani kutokana na kwamba hizi sehemu huwa na mafuta mengi.
Je utajuaje kama ni Skin Purging au Kipodozi hakija kupenda?
Skin Purging haikai muda mrefu lakini pia hutokea sehemu ambazo tayari zimeathirika mfano kama ulikuwa na chunusi kwenye paji la uso basi utaona zinazidi kutokea sehemu hio
Kipodozi Kutokukupenda huwa inatokea sehemu nyingine mbali na zile ambazo unatatizo lakini pia huchukua muda mrefu kupotea zaidi ya week sita.
Nini Cha Kufanya Endapo Ngozi Yako Inapitia Kipindi Cha Skin Purging
Unatakiwa kuendelea na routine yako kama kawaida na hakikisha upo consistent nayo bila ya kuacha, lakinipia huchukua week nne mpaka sita kuona matokeo unatakiwa kuwa mvumilivu.
Ni matumaini yetu umejifunza kitu.
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…