- Microblading ni nini?
Microblading ni cosmetic procedure ambayo huingiza rangi chini ya ngozi yako ya nyusi kwa kutumia sindano au mashine ya umeme na sindano. Microblading inakusudia kukupa well-defined eyebrows (nyusi) zilizoainishwa vizuri na kuonekana maridadi, procedure hii inasaidia kupunguza kuwa unapaka wanja kila siku, kwa maana rangi hii hukaa muda mrefu. Inawezakana kukaa kwa miezi 18-30.
- Imeanzishwa lini?
Procedure hii si mpya imekuwepo kwa takribani miaka 25 huko Asia na imekuwa ikitumika na maarufu nchini Merika na Ulaya, ndio maana unaweza kuona mtu maarufu kaamka na nyusi zake zimetindwa vyema tu.
- Je Hukaa Kwa Muda Gani?
Lakini rangi hii hupotea kama ambavyo tumesema inaweza kukaa kwa muda mrefu lakini pia inategemea na aina ya ngozi yako, kwa inavyosemekana, ukiwa na ngozi yenye mafuta sana inaweza isikae kwa muda mrefu kama wale ambao wanangozi kavu au mchanganyiko. Kiwango kikubwa cha sebum, au mafuta, yanayofichwa ndani ya ngozi yako inaweza kufanya iwe ngumu zaidi kwa rangi hii kukaa kwenye ngozi yako kwa muda mrefu.
- Ongea na mtaalam wako juu ya wasiwasi wowote ulio nao juu ya aina yako ya ngozi na ni muda gani unaweza kutarajia matokeo yako yatadumu.

- Inachukua Muda Gani Kupona?
Microblading inachukua siku 10 hadi 14 kupona na rangi kukaa katika umbo lake. Wakati wa mchakato huu, ngozi yako ya nyusi itakuwa sensitive, inakuwa laini na nyekundu kutokana na sindano kupita maeneo hayo.
Wakati mchakato wa kupona unaendelea usikune wala kushika kwenye eneo husika, endapo utafanya hivyo unaweza kusababisha vijidudu ambavyo vinaweza kunaswa chini ya ngozi yako na kusababisha maambukizo
Katika kipindi hiki cha uponyaji, unapaswa kuepuka kila aina ya unyevu kwenye nyusi zako. Hii ni pamoja na jasho kupindukia kutokana na kufanya kazi au kwa kuziloesha wakati unaoga bafuni au kwenye pool, kwa kifupi keep away any unyevu kwenye eneo hilo.
- Tahadhari na hatari
Kama unafikiria kufanya microblading, unapaswa kuzingatia hatari kadhaa:
Ukifanya Microblading tu, nyusi zako zitakuwa na rangi na umbo sawa hadi rangi iishe ( Kama ambavyo tulikua tunaona nyusi za Munah Love japo yeye alifanya tattoo) – ambayo inaweza kuchukua miezi 18 au zaidi. Kuwa na mashauriano ya kina na mtaalamu wako ambayo ni pamoja na kupitia jalada lao na kuwa na mchoro wa sura ya majaribio kwenye uso wako ili uweze kukagua namna utakavyokuwa kwa kipindi kirefu, yes miezi 30 ni sawa na miaka miwili na nusu.
Kutokana na kutumia sindano kufanya procedure hii unaweza kupata maumivu kwenye nyusi na endapo hutokuwa muangalifu kuweka eneo la nyusi safi na kavu basi unaweza kupata maambukizi ya sepsis na athari nyingine.
Note: kama unafikiria kufanya microblading, ni muhimu kufanya utafiti wako na kupata mtaalamu aliye na leseni, aliyekaguliwa vizuri, na anayeaminika
Related posts
3 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More Info here on that Topic: afroswagga.com/urembo/fahamu-zaidi-kuhusu-microblading-eye-brows/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on to that Topic: afroswagga.com/urembo/fahamu-zaidi-kuhusu-microblading-eye-brows/ […]
… [Trackback]
[…] There you can find 94636 more Info on that Topic: afroswagga.com/urembo/fahamu-zaidi-kuhusu-microblading-eye-brows/ […]