Manukato ndio kitu ambacho hufunga muonekano. Sio poa kabisa umependeza ila haunukii kama muonekano wako. Harufu huongeza kitu katika muonekano, inafanya uonekane unajijali na uko “put together” na wakati mwingine hukutambulisha. Ni muhimu sana kuwa makini na manukato hususani perfume. Perfume hutofautiana harufu na muda wa kudumu. Napoongelea harufu namaanisha harufu ambayo ukiingia sehemu watu wanaweza inusa bila kukusogelea kwa karibu sana.
Aina za perfume
Eau de Perfum
Katika chupa ya perfume aina hii, manukato ( chanzo cha harufu) ni asilimia 15 hadi 20. Huchukua muda mrefu zaidi kuisha mwilini yani masaa manne hadi matano mwilini.
Eau de Toilette
Hizi uwa na manukato asilimoa 5 hadi 15, mara nyingi hudumu kwa masaa mawili hadi matatu. Hizi ndio perfume zilizoenea na kuzoeleka zaidi. Watu wengi hutumia hizi perfume.
Eau de Cologne
Zina asilimia 2 hadi 4 ya manukato na alcohol nyibgi. Hudumu kwa masaa mawili na huwa na bei ndogo ukilinganisha na zilizotangulia.
Eau Fraiche
Hizi huwa na asilimia ndogo zaidi ya manukato yani asilimia 1 hadi 3. Pia ina alcohol kidogo na maji.Hudumu kwa muda mfupi zaidi mwilini.
Kuna sehemu kadhaa unaweza kupaka au kupulizia perfume. Ila katika hizi sehemu zote unapaswa kuchagua sehemu tatu za kupulizia unapotumia perfume, si vyema kupulizia sehemu nyingi sana. Pulizia perfume kwa kiasi tu, perfume nyingi sana kwa wakati sio nzuri. Pulizia au paka perfume yako nyuma ya magoti, kwenye kiungio cha mkono na kiganja kwa mbele, mbele ya kiwiko, nyuma ya masikio/shingoni/kwenye nywele , juu ya kitovu na pembeni ya miguu. Picha inaelezea zaidi
Vitu vya muhimu kujua kuhusu perfume
- Tunza perfume sehemu kavu isiyo na unyevunyevu
- Ili harufu idumu zaidi, paka vaseline sehemu unayitaka kupuliza.
- Ngozi yenye unyevunyevu hutunza manukato kwa muda zaidi hivyo paka kwenye ngozi isiyo kavu.
- Usisugue perfume au kuifuta na mkono baada ya kupaka.
- Kama harufu ni kali sana na unataka upate harufu kwa mbali tu basi puliza perfume hewani na kisha pita sehemu ulopulizia mara tu baada ya kupuliza.
- Perfume zenye alcohol hukausha ngozi na nywele. Badala ya kupuliza moja kwa moja kwenye nywele basi pulizia chanuo au kitana kisha pitisha kwenye nywele kama unachana.
- Unaweza kutumia perfume zaidi ya moja kutengeneza harufu ya tofauti.
- Ili kujua harufu halisi ya perfume subiri ikauke baada ya kupuliza ndio uinuse.
Haya ndio mambo muhimu zaidi kuhusu perfume. Siku nyingine unaponunua na kuchagua perfume basi ni muhimu kuyazingatia. Kama perfume zote hizi ni kali sana kwako unaweza kutumia aina nyingine za manukato kama body spray na splash.
Imeandaliwa na @style.with.mimie
Related posts
5 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More here to that Topic: afroswagga.com/urembo/fahamu-zaidi-kuhusu-perfume/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Information here on that Topic: afroswagga.com/urembo/fahamu-zaidi-kuhusu-perfume/ […]
… [Trackback]
[…] Read More to that Topic: afroswagga.com/urembo/fahamu-zaidi-kuhusu-perfume/ […]
… [Trackback]
[…] Information on that Topic: afroswagga.com/urembo/fahamu-zaidi-kuhusu-perfume/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on that Topic: afroswagga.com/urembo/fahamu-zaidi-kuhusu-perfume/ […]