Rangi za Gel zimechukua umaarufu mkubwa sana kwasasa hii imetokana na kwamba zimekuwa ni jibu la kilio kikubwa cha rangi kutoka mapema, rangi hizi hudumu kwa muda wa week mbili hadi tatu kama zikitunzwa vizuri, tofauti na rangi za kawaida ambazo hukaa kwa muda mchache.
Well ikiwa rangi hizi zimekuwa zikipakwa sana kwasasa kuna ambao wanazilalamikia na wale ambao wanazisifia, leo tunakuletea faida zake na hasara zake.:
Rangi ya Gel ni ipi?
Aina hii ya rangi imeundwa na methacrylate polymer, hii rangi hukaa muda mrefu katika kucha, rangi hii ni sawa tu rangi ya kawaida tofauti zake ni kwamba hii haikauki kawaida badala yake hukauka kwa kutumia ultraviolet au LED ya ultraviolet.
Faida za rangi ya Gel;
- Hudumu muda mrefu
Kama tulivyosema mwanzo rangi hizi huchukua muda kubanduka au kutoka, wakati mwingine hazitoki mpaka pale unapozichoka na kuamua kuzitoa mwenyewe.
- Zinakakuka kwa haraka
Sio kama rangi za kawaida zinaweza kuchukua muda mrefu kukauka na wakati mwingine design huharibika kabla ya kukauka, rangi hizi hukauka haraka kwa kutumia ultraviolet au LED ya ultraviolet.
- Nyepesi
Ukiachana na rangi nyingine ambazo unaweza kusikia uzito kwenye kucha, rangi za gel ni nyepesi mno.
Hasara za rangi za Gel
- Zinaweza kusabisha Cancer
Kumekuwa na report kwamba utumiaji wa kukausha rangi hizi si salama unaweza kusababisha ungonjwa wa cancer
- Husabaisha kucha kuwa dhaifu
Rangi hizi zimekuwa zikilalamikiwa kusababisha kucha za asili kudhoofika.
- Inaweza kusababisha maambukizo ( Infections)
- Wataalam wengine wanadai kuwa inachukua kucha karibu wiki 6 kupona baada ya kupaka rangi ya gel
Cha kufanya endapo utapaka rangi hii ya Gel:
- Pumzisha kucha baada ya kutoa rangi ya gel, husitoe ukapaka tena hakikisha zinapumzika kwa muda wa week kadhaa kabla ya kupaka tena rangi hii, kuzipaka mara kwa mara unazidi kudhoofisha kucha zako za asili
- Usikae nazo muda mrefu, rangi hii inaweza kudumu muda mrefu bila ya kuharibika lakini unashaurikwa kuitoa ndani ya week mbili hadi tatu usikae nazo zaidi ya hapo, sio tu zinaweza kudhoofisha kucha kwa kukaa nazo muda mrefu bali pia zinaweza kusababisha bakteria katika kucha.
- Nenda kwa mtaalamu kuondoa rangi hizi, inawezekana ukawa umezichoka na kuamua kutoa hii rangi mwenyewe, unashauriwa usitoe rangi hii kwa kubandua hakikisha unaenda kwa mtaalamu azitoe.
- Paka Sunscreen kwenye vidole vyako kabla ya kuingiza vidole vyako katika ultraviolet au LED ya ultraviolet, kulinda vidole vyako na mionzi hii ya kukaushia kucha.
Well ni matumaini yetu tumekusaidia.
Related posts
1 Comment
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More here to that Topic: afroswagga.com/urembo/fahamu-zaidi-kuhusu-rangi-za-gel/ […]