Kama ni mpenzi wa urembo utakuwa umeshakutana nayo au kusikia kuhusu retinol, Retinol inasifika kwa kuondoa mikunjo na kufanya ngozi irudi ujanan, well leo tunakuelezea kwa undani kuhusu retinol ni nini, inafanyaje kazi? na mengineyo.
Retinol ni nini?
- Retinol ni form ya vitamin A, ambayo hutumika kama kiungo kuwekwa katika cream, serum na lotion. Retional inasaidia kupambana na chunusi pamoja na uzee.
Umri Gani Unatakiwa Kuanza Kutumia Retinol?
- Inaaminika ngozi yako inaanza kuonyesha dalili za uzee kuanzia miaka 20, kwahio kuanzia miaka 20 au early 30’s unaweza kuanza kutumia.
Inatumika na jinsia gani?
- Jinsia zote zinaweza kutumia retinol.
Retinol Ina Faida Gani Katika Ngozi?
- Inaharakisha ubadilishaji wa seli (cell turnover), Inaharakisha mchakato wa ngozi yako ya asili kwakufanya cell turnover na kusababisha ngozi kufa haraka ili cell mpya zenye afya kuchukua nafasi yake.
- Inaongeza collagen, Collagen ni protini ambayo hufanya ngozi kuwa nene na dhabiti (yenye afya).
- Ina antioxidant properties ambayo husaidia kusaidia kupambana na radicals ambazo zinasababisha makunyanzi na madoa meusi
- Inasaidia kupambana na chunuzi, kwakuwa ina saidia kufanya cell turnover inasaidia kupambana na kuondoa whiteheads, blackheads, chunusi na pores zilizotokana na chunusi.

Namna Ya Kutumia Retinol
- Chukua drop moja kisha paka usoni na kwenye shingo, kama ambavyo inashauriwa unaweza kuanza kupaka mara moja kwa week, ukaongeza mara mbili kwa week unaweza kufanya hivi kwa mwezi kisha ukaanza kupaka kila siku baada ya ngozi kuzoea kipodozi.
Namna ya ku-introduce retinol katika skincare routine yako
- Cleanse
- Toner
- Retinol
- Moisturizer
- Sunscreen
Side effects za kutumia retinol
- Miwasho
- Ngozi kuwa kavu
- Ngozi kubabuka
- Kuwa sensitive na jua
Namna ya kukabiliana na side effects za retinol
- Anza taratibu kutambulisha retinol katika ngozi yako
- Paka sunscreen kupunguza ngozi kuwa sensitive na jua
- Punguza miwasho kwa kutumia soothing serums
- Paka moisturizer kupunguza ukavu wa ngozi
Inachukua muda gani kuona matokeo ya retinol?
- huwezi kuona matokeo ya retinol haraka huchukua week kadhaa baada ya kutumia kwa kawaida inaweza kuchukua hadi week 6 ndio uanze kuona matokeo yake.
Muda gani mzuri kutumia retinol?
- Kwakuwa retinol inasaidia kuharakisha cell turnover na ni sensitive kwa jua muda mzuri wa kutumia ni usiku na hakikisha unapaka sunscreen kesho yake.
Tahadhari:
- Usitumiee retinol kama unanyonyesha au ni mjamzito
- Usichanganye retinol na C, AHA, BHA, Benzoyl peroxide or any other active product
- Usiache kupaka sunscreen
Does Your Skin Break Out Before It Clears Up?
Namna Ya Kutambulisha Kipodozi Kipya Cha Ngozi Katika Ngozi Yako
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…