Bio oil ni mafuta yanayosifika sana na wengi hupenda kuyatumia! Leo utajifunza faida zake kama bado hujaanza kuyatumia fanya hivyo mara moja!
- Kuondoa Michirizi
Moja kati ya matumizi makubwa sana ya Bio-Oil ni kuondolea michirizi. Michirizi ni mistari inayotokea kwenye ngozi hususan tumboni na mapajani kutokana na ngozi kupoteza uwezo wake wa kuvutika.Matumizi sahihi ya Bio-Oil yanasaidia kupunguza ama kuondoa kabisa tatizo la michirizi katika ngozi

- Kuondoa Makovu
Bio-Oil husaidia sana kuondoa makovu, hususan itakapoanza kutumika mapema mara tu baada ya kidonda au jeraha kupona.Makovu machanga hupona haraka zaidi kuliko makovu ya muda mrefu
- Kutibu Ngozi Iliyosinyaa Na Kunyauka
Ndio. Kwa mtu mwenye ngozi iliyoanza kuzeeka au iliyozeeka basi atumie Bio-Oil. Baada ya muda sahihi ngozi yake itarejea hali ya uzuri na yenye afya
- Kutibu Ngozi Kavu / Iliyokauka
Bio – Oil inasaidia kuboresha afya ya ngozi na kuiwezesha iwe na maji na unyevu unyevu wa kutosha. Ngozi kavu huwahi kuzeeka, kwa hiyo matumizi ya Bio-Oil yatasaidia kuzuia ngozi kuwahi kuzeeka.

- Kurekebisha Rangi Tofauttofauti Za Ngozi Na Kuifanya Iwe Rangi Moja
Bio-Oil husaidia kurejesha afya ya seli za ngozi na kusaidia muonekano wake mzuri. Husaidia kuondoa rangi mbaya zisizopendeza zinazotokana na athari za jua, vipodozi, kuungua nk.Matokeo yake ni kuwa na ngozi nzuri yenye kupendeza, na rangi inayofanana.
- Bio Oil Inapatikana Wapi?
Bio-Oil hupatikana kwenye Famasi(Maduka ya dawa) na Maduka ya vipodozi.
Kuna changamoto kubwa sana ya Bio-Oil ambazo ni feki na zinapatikana kwa wingi hususan maduka ya vipodozi ambayo hayanunui kutoka kwa wasambazaji waaminifu.
Hakikisha Bio-Oil utakayonunua ni sahihi kwani ndipo utakapoona matokeo mazuri. Vinginevyo hautaona matokeo mazuri ilhali umetumia pesa nyingi sana kuyanunua.
Related posts
1 Comment
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More to that Topic: afroswagga.com/urembo/faida-na-matumizi-ya-mafuta-ya-bio-oil/ […]