Giligiliani ni kiungo cha kawaida sana,wengi tunakitumia jikoni kwenye mapishi mbalimbali,Kinaharufu nzuri na ladha ya uchachu kwa mbali.Majani na mbegu za giligiliani vyote hutumika kama viungo jikoni.Giligiliani inawingi wa Vitamini A, B6, C,B12,pia ina wingi wa madini chuma(iron),Calcium na Magnesium.
Giligiliani inasifika kwakua dawa na kinga ya magonjwa mengi.Historia inaonyesha kwamba Kiungo hiki kilitumika kama dawa tangu enzi za kale nchini Egypt. Hata hivyo,tafiti za kisayansi za karne hii ya 21 zinathibitisha taarifa hizi.
Ni vyema kujua kwamba tunaposema chakula Fulani ni dawa,basi maana yake ni kwamba chakula hicho kinavirutubisho Fulani ambavyo huweza kukabiliana na ugonjwa Fulani au laa kuupa mwili uwezo wa kukabiliana na kujikinga na ugonjwa Fulani na si vinginevyo.
Hizi ni baadhi ya faida za giligiliani katika Urembo :
1. Huondoa chunusi na madoa kwenye ngozi.
Mahitaji
- Giligilani kiasi
- Kijiko kimoja cha Manjano (Binzari Manjano)
Ili kuondoa chunusi na madoa meusi. Twanga au sigina majani ya giligiliani, chuja au kamua ili kupata maji yake. Pima vijiko vinne vya maji ya giligiliani kisha changanya na kijiko 1 cha chakula cha manjano(Binzari manjano).Pakaa kwenye ngozi ,acha ikauke kisha osha au nawa na maji vuguvugu.
Onyo: Usisugue ngozi paka taratibu
Kuipa ngozi mng’ao.
Mahitaji
- Giligilani kiasi
- Tango 1
Saga giligilani na tango pamoja upate mchanganyiko mzito, hii utatumia Kama mask. Pakaa usoni Baki nayo kwa dakika 20 Kisha Osha kwa maji ya kawaida.
Rudia Kwa wiki Mara moja Sio zaidi ya Mara mbili.
Mask hii Inatumika kwa ngozi aina zote Ila ni nzuri zaidi Kwa wenye Ngozi ya mafuta.
Jee wewe unatumiaje giligilani kwenye Urembo!? Tuambie kwenye comment hapo chini
Shea na uwapendao , imeandikwa na @binturembo
Related posts
6 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Information on that Topic: afroswagga.com/urembo/faida-za-giligilani-coriander-kwenye-urembo/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Info here to that Topic: afroswagga.com/urembo/faida-za-giligilani-coriander-kwenye-urembo/ […]
… [Trackback]
[…] Info to that Topic: afroswagga.com/urembo/faida-za-giligilani-coriander-kwenye-urembo/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Info here on that Topic: afroswagga.com/urembo/faida-za-giligilani-coriander-kwenye-urembo/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Information here to that Topic: afroswagga.com/urembo/faida-za-giligilani-coriander-kwenye-urembo/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on on that Topic: afroswagga.com/urembo/faida-za-giligilani-coriander-kwenye-urembo/ […]