Lipstick ni aina ya vipodozi vyenye rangi mbalimbali vinavyotumika kupaka katika midomo hasa ya wanawake ili kuongeza urembo na mvuto wao. Historia ya kupaka rangi kwenye midomo kwa kusudi la urembo inaonyesha kuwa jambo hili lilianza zamani sana na inasemekana kuwa lilianzia huko Misri .
Ingawa matumizi ya rangi ya kupaka midomoni katika siku zetu inaweza kuwa na makusudi tofauti na yale ya zamani na kupendwa na wasichana au wanawake wa kisasa wanaokwenda na wakati katika urembo, lakini bado ni muhimu kuangalia athari zake kwa afya ya jamii na mwili wa mtumiaji mwenyewe.
Vipodozi hivi hutengenezwa kutokana na viambato mbalimbali na inasemekana kuwa baadhi ya viambato hivyo si salama kwa afya.
Watafiti wa mambo ya afya ya jamii wanasema kuwa wanawake wengi wanaotumia rangi za kupaka midomoni wanachoangalia zaidi ni urembo na mvuto wao na wanasahau kuangalia upande wa pili wa athari zake kwa afya zao.
Katika utafiti uliofanywa huko Marekani na US Consumer Group “Campain for Safe Cosmetics” Oktoba 2007, ripoti yao iliyopewa jina la “A Poison Kiss, the Problem of Lead in Lipstick” (Busu lenye sumu) ilionyesha kuwa lipstick nyingi karibu theluthi moja, zilikuwa na madini ya ‘lead’ kwa kiwango kikubwa zaidi ya kile kilicho salama kwa afya ya binadamu.
Viambato vingine vyenye madhara ambavyo vinapatikana katika rangi hizi kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari za afya ya jamii ni pamoja na Butylated Hydroxyanisole (BHA), Coal tar (petroleum) na aluminum (Lakes color).

Lakini pia ndani ya rangi za kupaka mdomoni kuna rangi ya Carmine au natural red 4, rangi inayotokana na wadudu wekundu waliokaushwa na kusagwa kama vile ‘Red Beetles’.
Pamoja na rangi hii, baadhi ya vipodozi hivi pia huongezewa mafuta ya nguruwe au mafuta ya ubongo wa ng’ombe kama malighafi za kutengenezea vipodozi hivi ili viweze kulainisha midomo. Watengenezaji wengine huongeza rangi za magamba ya samaki pamoja na mazao ya mimea kama vile red beets na bizari. Mdudu RED BEETLE anaye tumika kutengenezea Lip stick
- MADHARA YA MATUMIZI YA LIPSTICK.
Wanasayansi wanaongeza kusema kuwa viambato vyenye madhara katika rangi za kupaka midomoni vinaweza kuingia mwilini au kumezwa na kusababisha athari za kiafya kama vile saratani (kansa), magonjwa ya figo, shinikizo la damu, uchovu wa mwili usiokuwa na sababu bayana, kukosekana kwa usawaziko wa kihisia (mood swing), maumivu ya kichwa, kichefuchefu, magonjwa ya ngozi, kupasuka kwa midomo (cheilitis) na magonjwa ya neva.
Matatizo mengi ya kiafya yanayosababishwa na rangi hizi, hayatokei kwa haraka na ni mara chache sana waathirika wa rangi hizi kuhusisha utokeaji wa magonjwa wanayopata na mtindo wao wa maisha wa kutumia vipodozi hivi.
Wanawake wajawazito wanaotumia vipodozi hivi, huwaweka watoto wao walioko tumboni katika hatari ya kupata magonjwa wa mtindio wa ubongo na matatizo ya akili [Utaahira].
Sumu ya lead inayopatikana katika baadhi ya vipodozi hivi hupita katika kondo la nyuma na kufika katika ubongo mchanga wa watoto walioko tumboni na kuathiri maendeleo ya ubongo na akili za mtoto, na matokeo yake ni kuzaa mtoto asiye na uwezo wa kuelewa kile anachofundishwa kwa haraka.
Wasichana na wanawake wanashauriwa kujiepusha na matumizi ya rangi hizi kwa ajili ya kulinda afya zao. Lakini kama hakuna njia nzingine zilizo salama zaidi za kukamilisha urembo wako, unashauriwa kuepuka kujilambalamba midomo pale unapokuwa umepaka rangi hizi mdomoni.Hii hupunguza kiasi cha viambato hatarishi vinavyoingia mwilini kwa njia ya kumeza, ingawa kiasi kingine kinaweza kupenya kupitia katika ngozi laini ya midomo na kuingia ndani ya damu.
Tumia lipstick kwa uangalifu, Shea na uwapendao.
©binturembo
Related posts
4 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More to that Topic: afroswagga.com/urembo/historia-na-madhara-ya-lipstick-kwa-wanawake/ […]
… [Trackback]
[…] There you will find 1053 more Information on that Topic: afroswagga.com/urembo/historia-na-madhara-ya-lipstick-kwa-wanawake/ […]
… [Trackback]
[…] Info on that Topic: afroswagga.com/urembo/historia-na-madhara-ya-lipstick-kwa-wanawake/ […]
… [Trackback]
[…] Info to that Topic: afroswagga.com/urembo/historia-na-madhara-ya-lipstick-kwa-wanawake/ […]