Wengi hudhani kujali ngozi ni kupaka mafuta au kutumia skin careĀ lakini kumbe kuna vitu vichache ambavyo tuna visahau kufanya na ni muhimu sana, vitu hivyo ni kama;
Badilisha foronya za mito unayolalia.
Tunapo lalia foronya kuna bacteria wengi ambao tunawaacha hivyo hata kama ukiwa una paka mafuta mazuri kiasi gani unapo rudi kulala kwenye ile foronya lazima ngozi itaharibiwa tena na wale bacteria, badilisha foronya za mito mara mbili kwa wiki.
Safisha Makeup Kits Zako Mara Moja Kwa Week
Kama ilivyo kwa mito basi pia ni hivyo hivyo katika make up brushes jaribu kuzifanyia usafi mara moja katika kila wiki na utaona matokeo mazuri katika ngozi yako.
Safisha Uso Wako Kabla Ya Kulala
Hakikisha unaosha uso wako kwa maji masafi na sabuni kila siku kabla ya kwenda kulala, hii husaidia kuacha ngozi yako safi, kuondoa bacteria wa siku nzima na kufungua matundu yaliyo jaa vumbi au mafuta ya mwilini.
Kunywa Maji Mengi
Maji ni huduma kubwa sana kwa afya sio ya mwili tu bali ya ngozi pia, jaribu kubeba chupa ya maji na unywe mara kwa mara utaona matokeo ya jinsi ambavyo ngozi yako itakavyo nawili.
Epuka Kutumia Vipodozi Vyenye Kemikali Nyingi
Kuna chemicals/kemikali ambazo zinaharibu ngozi, jaribu kutumia vitu vya asili kama mayai, asali au hata limao pia husaidia.
Acha Kutumbua VipeleĀ
Acha kutumbua vipele, kutumbua vipele unaweza kusababisha vidonda au madoa usoni jaribu kupaka dawa sehemu yenye kipele kuna njia nyingi kama dawa ya mswaki au hata limao inaweza kukausha kipele bila kuaharibu ngozi.
Related posts
1 Comment
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Information to that Topic: afroswagga.com/urembo/jali-ngozi-yako-kwa-kufanya-haya/ […]