Kwasasa skincare products ambazo zinasifika kwa uwezo wake wa kufanya ngozi kuwa nzuri na kuondoa breakout ni vipodozi vya kikorea, ambavyo inasemekana vipodozi hivi hutengenezwa asilimia kubwa na vitu vya asili na vitu ambavyo havina madhara lakini pia vinasifika kwa kuleta unywevu katika ngozi.
Japo vipodozi hivi ni vizuri na Dunia inavisifia haimaanishi basi haviwezi kukusababishia madhara katika ngozi inawezekana vikaleta madhara kama vipodozi vingine mfano:
- Korean Skincare ni tofauti kidogo wana routine mpaka ya vipodozi 10, kama ngozi yako haijazoea na kama umenunua tu bila mpangilio na kujua kipodozi gani ninaendana na kipodozi gani basi unaweza kupata madhara.
- Pia kuna active ingredients katika vipodozi vyao, kama uso wako haujazoea ingredients hizi pia inawezekana kupata madhara.
- Endapo utanunua kipodozi bila kujua kama kinaendana na ngozi yako au lah, sababu tu ni Korean product haimaanishi inafaa kwa kila aina ya ngozi japo vingi vinaandikwa hivyo lakini ni vyema kujua aina ya ngozi yako na kipodozi kipi kinakufaa.
- Kama unafikiria kufuata utaratibu wa utunzaji wa ngozi wa Kikorea, ni muhimu kufanya utafiti wako na kupata bidhaa zinazofaa kwa aina ya ngozi yako. Anza na kiasi kidogo cha bidhaa na ongeza kadri ngozi inavyozizoea.
- Japo vipodozi hivi vinasifika lakini tukumbuke pia swala la ngozi linatokana na unachokula pia, tunapoona wa Korea wana ngozi nzuri pia wanakula vyakula vizuri na hii inaonekana hata kwenye life span yao ni ndefu kuliko sisi, kama unatumia kipodozi cha kikorea na una kula vyakula visivyo sahihi basi pia unaweza usione matokeo mazuri.
Tuambie je ulishawahi kutumia vipodozi hivi na matokeo yake yalikuwaje?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…