Tunatumia muda mwingi katika kuhakikisha ngozi zetu zinakuwa nzuri, unakuwa na skin care routine, unaosha uso wako vyema lakini bado utakuta matokeo hayawi vile ambavyo unategemea kumbe kuna baadhi ya vitu vidogo vidogo ambavyo vinasababisha hili kimoja wapo ikiwa ni Taulo, Khanga, Kitenge au kitu chochote ambacho unatumia kufutia mwili wako pamoja na uso wako.

- Swali Je naweza kutumia taulo moja usoni na mwilini?
Jibu ni HAPANA ni vyema kuwa na mataulo tofauti ya kujifutia usoni na mwilini. kama ambavyo tunajua taulo linapita sehemu nyingi kujifutia ikiwepo miguuni na sehemu nyeti kuna bacteria ambao unaweza kuwatoa sehemu moja na kupeleka nyingine ikaleta madhara.
- Je Ni Kwa Kipindi Gani Nahitajika Kusafisha Taulo / Kitambaa Cha Kufutia Uso?
Unatakiwa kukisafisha kitambaa hiki mara kwa mara unapokitumia, au kutumia kipya mara baada ya kutumia kwa muda fulani eg siku mbili. Lakini hakikisha pia taulo, khanga, kitenge chako kinakauka kabla ya kukitumia tena na hii sio tu kwa kitambaa cha usoni bali hata mwilini.
- Je Ni Kitambaa Cha Aina Gani Kinafaa Kutumia Kama Face Towel?
Kitambaa chochote ambacho ni laini, kitambaa kigumu kinaweza kusababisha michubuko, kupata wekundu katika ngozi na madhara mengine hakikisha kitambaa unachotumia ni soft na hakitaleta madhara yoyote katika ngozi yako.
MUHIMU: kama unaona kufua au kubadilisha kitambaa chako cha usoni mara kwa mara ni shida kwako basi acha uso wako ukauke kwa hewa huitaji kitaulo kukausha, hii tu sio inasaidia kuepusha usumbufu wa kufua na kubadilisha kitambaa lakini pia hufanya ngozi yako kuwa hydrated kwa sababu ngozi inanyonya maji.
Related posts
HOT TOPICS
As long as hakuna Aya,Mstari Au Kifungu Kinachosema “Kuto Kuoga Ni Dhambi Au Kosa Kisheria” Then Perfume na Bodyspray Tu Zinatosha Msimu Huu
FollowDown To Very Little Details, Read More Here 👇🏾👇🏾👇🏾👇🏾👇🏾 https://t.co/IeYufSGMgy https://t.co/IeYufSGMgy
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…