Kupaka makeup kumekua ni kitu cha kawaida na kinachopendelewa na watu wa rika tofauti. Kuna mbinu mbalimbali za kufanya makeup na moja wapo ni Contouring na leo make up artist @flawlessfacesbysoso anakuletea mbinu hizo za kupaka contour
Contouring ni moja ya mbinu ya kufanya make up ambayo ni mahsusi kwa ajili ya kuchonga baadhi ya sehemu ya uso na kuifanya sura kuwa defined zaidi na pia kubadili muonekano wa viungo kwa usoni kutegemea na jinsi mtu anavyopenda. Mfano kuchonga pua ionekane nyembamba zaidi ya ilivyo, lips zionekane kubwa zaidi au hata sura ionekane nyembamba au nene kuliko kawaida. Hii inategemea na mapenzi ya mtu na jinsi gani anataka aonekane.
Kama inavyojulikana, kila mtu ana rangi yake ya mwili. Mbinu hii ya contouring inabidi kutumia foundation ama concealer ambayo ni ya giza zaidi kuliko rangi ya mwili wako ama ile ambayo inafanana na foundation uliyopaka mwanzoni (foundation inatakiwa ifanane na rangi ya ngozi).
Countouring inaenda sambamba na highlighting, ambapo kwenye highlighting inatumika concealer ambayo ina nuru (light) mara moja au mbili zaidi ya rangi ya ngozi yako. Hii yote hi kuweka mwanga baadhi ya sehemu ya uso.
Hizi ni sehemu contour inapofanyika na jinsi inayoweza kubadili sura:
Pua: Inafanya pua ionekane ndefu zaidi. HaipendezI kuzidisha sana contour kwenye pua maana itapoteza uhalisia.
Kwenye mashavu/Cheekbones: inafanya sura ionekane nyembamba zaidi.
Taya (Jaw): uki Contour taya inashape sura na kufanya mtu alieongezea unene wa sura kuonekana nyembamba na kuchonga zaidi.
Sehemu nyingine ni kama zinavyoonekana kwenye picha, wapi pa ku highlight na wapi pa kucontour
Ni muhimu pia kujua muundo wa uso wako kwa kabla haujafanya Countoring na Highlighting. Hii ni kwasababu sura zinatofautiana muundo.
Jinsi Ya ku-Contour kulingana na muundo wa sura yako
Cha muhimu pia wakati wa contouring na highlighting ni ku blend (kuchanganya) vizuri concealer uliotumia pale unapoipaka usoni kwa kutumia beauty blender au brush, ili kuzuia sura isionekane kama ina matope na kuleta uhalisia wa sura yako.
Related posts
HOT TOPICS
We need to have some sort of bima ila for enjoyment. Yaani wanakata ka % ka mshahara kako unakua na card ukienda se… https://t.co/W9oDoaN2YY
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…