Kuna watu ni wazuri jamani ila uzuri wao hauonekani sababu ngozi zao zipo rough sana, ubora wa ngozi ni matokeo ya mambo mengi sana ,najua kufanya yote kwa sisi tulio busy ni ngumu kidogo , ila ukifanya japo mawili matatu utanawirika tu.
Nakukumbusha mambo hayo ya msingi ni kula vizuri mbogamboga na matunda, kunywa maji mengi na kusafisha uso kwa vitu asilia angalau mara moja kwa wiki. Zipo njia nyingi sana za kusafisha ngozi kiasili. Leo nitakupa moja na ukiifanya ipasavyo haitokuangusha.
Nitatenganisha jinsi ya kusafisha ngozi ya mafuta na zile ngozi za kawaida na kavu. Kama huijui aina ya ngozi yako , Soma andiko hapo chini litakusaidia
KWA NGOZI YA MAFUTA
Mahitaji
- Ute wa yai
- kipande cha limao
- manjano kijiko kimoja
Jinsi ya kufanya
- Changanya vitu vyote katika chombo kimoja
- kisha osha uso na sabuni isiyo na kemikali
- jikaushe kisha paka mchanganyiko wako usoni kaa nao kwa dakika 20 hadi 30 kisha osha
- Ili kuzuia ngozi isiwe kavu Sana ,paka moisturizer unayotumia.

KWA NGOZI KAVU NA YA KAWAIDA
Mahitaji
- Kiini cha yai
- maziwa fresh
- Manjano kijiko kimoja
Jinsi ya kufanya
- Changanya vitu vyote katika chombo kimoja
- kisha osha uso na sabuni isiyo na kemikali
- jikaushe kisha paka mchanganyiko wako usoni.kaa nao kwa dakika 20 hadi 30 kisha osha.
Ili kuzuia ngozi isiwe kavu Sana ,paka moisturizer unayotumia.
Related posts
1 Comment
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More here to that Topic: afroswagga.com/urembo/jinsi-ya-kupata-ngozi-mtelezo-flawless-skin/ […]