Tango ni tunda muhimu sana katika kusaidia afya na uzuri wa ngozi. Unaweza kula tunda lenyewe, kupaka juisi yake, kugandika vipande vyake vidogo vidogo au kunywa juisi yake. Njia zote hizo zinakusaidia kupata virutubisho muhimu kwa ngozi yako.
Tango husaidia sana kulainisha ngozi na kuikaza ngozi iliyonyauka na kulegea. Yaani hufanya kazi ya Skin Tonning ya asili. Pia ukiitumia kwa muda endelevu husaidia kuondoa na kuzuia chunusi kubwa kubwa (Pimples), makovu ya chunusi, makunyanzi na ukavu wa ngozi ya usoni.
Ni moja kati ya tunda muhimu sana kwa ajili ya matundo na upendezeshaji wa ngozi yako.
Jinsi Ya Kuandaa Na Kutumia Tango Vizuri
- Andaa tango, maji, chombo cha kuwekea vipande vya tango na kifaa cha kukatia tango (Grater) lako katika vipande vidogo vidogo na laini Osha tango lako, chombo chako na kifaa chako cha kukatia tango lako.
- Bila kumenya, anza kulikatakata tango lako katika vipande vidogo vidogo sana na laini na kuweka kwenye chombo chako Ukimaliza kukata tango lako chukua vipande hivyo vidogo vidogo na laini kisha paka usoni, kuzunguka macho na shingoni pamoja na juisi yake
- Acha ikae kwa dakika 15 – 20 na kisha nawa kwa maji na uache bila kujikausha.
- Rudia hivyo kila siku na kwa muda endelevu hadi matokeo yatakapokuwa mazuri
Faida Za Kufanya Hivi Ni
- rahisi sana na salama
- Ufanisi wake ni mkubwa
- Gharama yake ni nafuu
Ushauri
- Tumia matango mazuri na kata kata vizuri vipande vyako.
- Hakikisha unatumia mara tu baada ya kutengeneza, usilaze wala kutumia vipande vilivyolala. Kuwa mvumilivu kidogo, utaanza kuona matokeo mazuri baada ya wiki mbili.
- Kama unapenda vipodozi vya asili basi tango ni zuri sana kwako. Kula tango, kunywa juisi ya tango, paka vipande na juisi ya matango.
Related posts
2 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] There you can find 67406 more Information on that Topic: afroswagga.com/urembo/jinsi-ya-kutumia-tango-kuilainisha-ngozi/ […]
… [Trackback]
[…] Find More to that Topic: afroswagga.com/urembo/jinsi-ya-kutumia-tango-kuilainisha-ngozi/ […]