Week iliyopita tulipata kujua kuhusu namna ambavyo unaweza kutunza ngozi yako, ambapo tulianza na kuongelea kuhusu cleansing, lakini kuna step tatu ambazo inabidi uzifuate katika utunzaji wa ngozi yako kila siku nayo ni Cleanser, Tonning na Moisturizing. Leo tutajua face toner ni nini na namna ambavyo unaweza kufanya face toner.
Face toner is basically an in-between skin-care step, baada ya kuosha uso wako kabla ya kupaka mafuta (moisturizer) step inayofuata ndio huitwa facial toning, zimetengenezwa kwa ajili ya ku-re-balance skin baada ya kuosha uso wako kwa kutumia sabuni kali au cleanser, yaani hii huifanya ngozi yako irudi katika hali yake ya awali baada ya kuiosha na sabuni au cleanser zenye kemikali na kabla hujapaka mafuta.
Toners ni muhimu zaidi kwa watu walio na ngozi ya mafuta, au watu wanaotumia vitu vya ziada kama makeup au bidhaa nyingine za ngozi kama sun screen, lakini pia zipo kwa ajili ya kila aina ya ngozi kama ngozi kavu, sensitive skin na aina nyingine za ngozi, cha muhimu ni kujua aina ya ngozi yako na kujua toner ipi inakufaa.
Faida Nyingine za Toner Ni
- Inarudisha usawa wa Hp katika ngozi yako
Kawaida ngozi yetu ni acidic, pH balance katika ngozi zetu ni kati ya tano na sita (kwa kiwango cha 0 hadi 14). Lakini usawa huo unaweza kutolewa baada ya kuosha ngozi zetu kwa kutumia sabuni zenye kemikali kali, ili ngozi kurudi katika hali yake ya kawaida huchukua muda kidogo lakini kutumia toner inaweza kusaidia kurejesha usawa huu haraka.
-
Inaongeza safu ya ulinzi katika ngozi.
Toner husaidia kuziba mashimo ya chunusi au yaliyo achwa wazi baada ya kuosha uso wako, hii husaidia kupunguza kupenya kwa uchafu katika matundu hayo na kusababisha uharibufu wa ngozi kwa chunusi au magonjwa ya ngozi.
- Husaidia kupunguza mafuta kwenye ngozi mafuta, na kuongeza unyevu kwenye ngozi kavu
kwa ngozi ya mafuta inaweza kuwa na viungo vinavyopunguza uzalishaji wa mafuta, wakati toner kwa ngozi kavu inaweza kuwa na viungo vingi vya maji na kusaidia kuongeza unyevu katika ngozi yako.
Namna Ya Kutumia Face Toner
Kutumia face toner ni rahisi sana, unaweza kutumia pamba kwa kumiminia face toner kwenye pamba na kupaka usoni, kwenye masikio ,shingo na kifua, au kwa kutumia viganja vyako vya mikono. unapaswa kutumia toner baada ya kuosha uso wako, na kabla ya kutumia serum au moisturizer.
Toners inaweza kutumika mara mbili kila siku baada ya kusafisha uso wako.
Related posts
1 Comment
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Info on that Topic: afroswagga.com/urembo/jinsi-ya-kutunza-ngozi-kilasiku-skin-care-routine-2/ […]