SUBSCRIBE NOW

* Afromate kuwa wakwanza kupata updates zetu za kila siku!

Trending News

Subscribe Now

* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!

Trending News

Jinsi Ya Kutunza Ngozi Kilasiku ( Skin Care Routine) – 3
Skin Care

Jinsi Ya Kutunza Ngozi Kilasiku ( Skin Care Routine) – 3 

leo tupo kwenye hatua ya mwisho ya skin care routine, ambapo tulishaangalia kuhusu cleanser, Tonning na leo tupo kwenye step ya mwisho iitwayo moisturizing ( hapa ni kuipa ngozi yako unyevu). Hii ndio step ambayo wengi wetu tunaijua na kuipenda sana, tatizo letu kubwa ni kutokujua nini tutumie kama moisturizer (mafuta ya ngozi), mara nyingi tunatumia watu kuuliza wanatumia kipodozi gani na sisi tunaenda kununua hikohiko na kukitumia bila kujali labda mwenzio ana aina tofauti ya ngozi na yako.

Jambo la kwanza unalotakiwa kujua ni aina ya ngozi yako na vipodozi gani vinakufaa, Kila aina ya ngozi inavipodozi vyake na ni tofauti na aina nyingine ya ngozi. Ukishajua aina ya ngozi uliyo nayo jaribu kuangalia ingredients na expiration date ya kipodozi hiko, usinunue tu bila kuangalia vitu hivi viwili unaweza kuwa na allergy nacho au kama ime expire unaweza kupata matatizo ya ngozi.

Kwanini upake mafuta ngozi yako? 

  • Mafuta husaidia kuilinda ngozi yako na mazingira

Unaweza kusangaa ngozi ilindwe na mazingira? yes unapo paka mafuta yana virutubisho vya kuzia jua hii husaidia kukuepusha na kuharibika kwa ngozi, vumbi ambazo zikiingia kwenye ngozi husababisha chunusi na husaidia kukulinda na mazingira mengine hatarishi ambayo yanaweza kuharibu ngozi yako

  • Kuipa ngozi yako afya

Katika mafuta kuna virutisho mbalimbali ambavyo husaidia kujenga ngozi yako, kuipa afya, kuifanya iwe nyororo, comfortable na attractive kama wewe ni mmoja kati ya ambao unaulizwa unatumia kipodozi gani basi jua ni kwasababu ngozi yako ina afya na inavutia.

  • Kuipa ngozi unyevu

Mafuta husaidia kuipa ngozi yako unyevu ambao  husaidia kulisha na kuboresha ngozi yako kwa njia kadhaa kama

Kuondoa mafuta na kuifanya ngozi yako iwe nzuri kwa asili

Kufunika na kulinda fissures ndogo katika ngozi yako

Inajenga safu ya ulinzi wa kulinda ngozi kutoka mazingira yenye uharibifu

Tumemaliza kuhusu njia tatu za kutunza ngozi yako kila siku kama kuna mada ambayo ungependa iongelewe baada ya hii usisite kutuandikia hapo chini, kama ulipitwa na njia ya kwanza na ya pili tumekuwekea link hapo chini pia..

Related posts

5 Comments

  1. pg사

    … [Trackback]

    […] Read More Information here to that Topic: afroswagga.com/urembo/jinsi-ya-kutunza-ngozi-kilasiku-skin-care-routine-3/ […]

  2. 코인커뮤니티

    … [Trackback]

    […] Info to that Topic: afroswagga.com/urembo/jinsi-ya-kutunza-ngozi-kilasiku-skin-care-routine-3/ […]

  3. ประตู wpc

    … [Trackback]

    […] Read More here to that Topic: afroswagga.com/urembo/jinsi-ya-kutunza-ngozi-kilasiku-skin-care-routine-3/ […]

  4. bonanza178

    … [Trackback]

    […] Here you can find 93140 additional Info on that Topic: afroswagga.com/urembo/jinsi-ya-kutunza-ngozi-kilasiku-skin-care-routine-3/ […]

Comments are closed.