Mlipuko wa ugonjwa wa Corona ( COVD 19) umeathiri Mataifa mbali mbali ikiwemo Tanzania. Hali hii imesababisha ratiba na mwenendo wa maisha kubadilika. Hapa chini tunakuletea jinsi unavyoweza kutunza ngozi yako wakati huu wa COVD-19
- Kaa mbali na Msongo wa Mawazo.Ugonjwa wa Corona upo, unatia hofu na ukifikiria sana unaweza kupata msongo wa mawazo na usijue cha kufanya na kuongeza hofu zaidi hii sio tu itaathiri kinga ya mwili wako bali hata afya ya ngozi yako na mwili kwa ujumla. Zuia vyanzo vyote vya msongo kama vile vyanzo vya taarifa zisizoaminika, anaekutumia ama wewe mwenyewe kwa kufatilia. Acha kufatilia vyanzo visivyoaminika kwa kuwa vitakuongezea hofu na mengine yatatokea yaliyotajwa hapo juu.
- Fuata ushauri wa wataalamu kama wanavyosema na endelea kuchukua tahadhari. Afya tako ni muhimu, ukiwa na afya njema hio inahusisha na ngozi yako pia.
- Vaa barakoa. Hii ni muhimu sana hasa unapotoka kwenda kwenye safari zako za lazima. Lakini ni muhimu sana kuvaa barakoa nusu saa baada ya kufanya skin care routine yako. Na usirudie kuvaa barakoa kama hujaifua / kuisafisha kwa zile zenye sifa ya kufuliwa. Ambazo hazina sifa hizo zitupe na kuziteketeza kama maelezo yanavyotolewa. Kurudia barakoa iliyo chafu sio tu itakuongezea shambulio la chunusi bali hata kukuweka kwenye hatari ya kupata maambukizi mengineyo. Usirudie Barakoa!
- Nawa mikono mara kwa mara kwa kutumia maji tiririka na Sabuni. Baada ya kunawa paka hand cream/ hand lotion/ hand moiturizer/ hand oil kuzuia ukavu. Hizi zinaongeza unyevu kwenye ngozi, hasa kama wewe unapata ukavu baada ya kutumia moisturizer, paka hand cream yako ukavu utaondoka.

- Changamoto ya skin care routine na barakoa.Kama una safari basi fanya routine yako nusu saa kabla ya kuvaa barakoa na usirudie kuvaa barakoa.
- Jitahidi kuwa off make up kuzuia congestion ya materials kwenye ngozi yako. Ufanye routine yako upake make up kisha uvae barakoa unaweza kuona ni jinsi gani inaweza kuwa changamoto kwako. Chagua kuwa off make up. Kama ni lazima kupaka make up, tumia original products na utakaporejea osha make up yako kabla ya kulala na ukumbuke kufanya skin care riutine yako ya usiku. Na ile barakoa yako ioshe pia na kama ni ya kutupa itupe kama inavyotakiwa ama kuichoma moto.
- Barakoa za kufua, fua kabla ya kuzivaa tena. Na upige pasi kuhakikisha unaua wadudu mbali mbali ambao si tu wataathiri afya ya ngozi yako hadi afya yako kwa ujumla.
- Kama si lazima kutoka nje ya nyumba yako baki nyumbani na uendelee kuwa salama kutokana na hali ya huko nje pamoja na jua. Kama kuna ulazima wa kutoka nje ya nyumba yako, Chukua tahadhari ya kuepuka mikusanyiko, kuepuka kusalimiana kwa kupeana mikono, kuepuka kukaa karibu na watu na kutumia vitakasa mikono ” sanitizer”.
- Usiache kutumia sunscreen. Sunscreen ni muhimu sana, uwe unaenda nje, au hauendi uwe unatoka au hutoki. Endelea kufanya skin care routine yako kama kawaida na Usiache kutumia sunscreen.
Jilinde na uwalinde wengine, Baki Nyumbani ubaki salama.
Jee wewe unafanya nini zaidi kuendelea kuwa na ngozi yenye afya wakati huu wa COVD 19 ?
Shea na sisi kwenye comment!
Related posts
4 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More here to that Topic: afroswagga.com/urembo/jinsi-ya-kutunza-ngozi-yako-wakati-huu-wa-covd19/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on that Topic: afroswagga.com/urembo/jinsi-ya-kutunza-ngozi-yako-wakati-huu-wa-covd19/ […]
… [Trackback]
[…] Find More to that Topic: afroswagga.com/urembo/jinsi-ya-kutunza-ngozi-yako-wakati-huu-wa-covd19/ […]
… [Trackback]
[…] Find More Info here on that Topic: afroswagga.com/urembo/jinsi-ya-kutunza-ngozi-yako-wakati-huu-wa-covd19/ […]