Lipstick ni kipodozi chenye rangi ambacho mara nyingi upakwa mdomoni na ipo katika muundo wa kimti (lip-mdomo, stick-mti).
Lipstick zipo za aina na rangi na zina faida tofauti tofauti kwanza tutaanza na aina za lipstick,
Lipstick kavu – hizi hazina mafuta kabisa ukipaka zina kaa kwa muda mrefu sana na pia hufanya upate muonekano natural na bold. kwa sasa ndizo hutumika sana
Lipstick za mafuta – hizi ni zile zenye mafuta hazichukui muda kufutika, lakini ni nzuri kwa ngozi ya midomo yako hasa kwa wale wenye midomo mikavu husaidia kuto kubabusha ngozi. Kwa sababu hizi ndizo zilikua za kwanza kabla ya kavu ndani yake kuna aina mbali mbali za lipstick lakini zote kwa ujumla uitwa lipstick za mafuta.
Faida za Lipstick kuna faida mbali mbali za kupaka lipstick baadhi yake ni:
uzuri- lipstick zinakupa muonekano mzuri usoni, ukiwa umepaka lipstick ya rangi yoyote ile ina kuongezea uzuri wako katika uso pia kama una hitaji kusimama mbele za watu au una hitaji kujiongezea kujiamini basi Lipstick ndio jibu lako.
Kuipa midomo yako unyevu – kutokana na kuwa na mafuta na baadhi ya kemikali zenye mafuta na afya Lipstick zina saidia kuipa midomo yako unyevu ambao husaidia kuto kuharibika kwa midomo yako (mf; kubabuka midomo).
Jua – midomo ipo usoni kuikinga na jua ni kazi sana ni hadi uvae kofia lakini ni vipi endapo sehemu unazo tembelea mara kwa mara hazikuruhusu wewe kuvaa kofia? ni vyema ukapaka lipstick ili kuzuia midomo yako kuharibika na jua, baridi au hata upepo ambapo vitu hivi vinaweza kuiletea midomo yako madhara.
lipstick zina kemikali mbali mbali ambazo zinaweza kusaidia kuikinga midomo yako na baadhi ya magonjwa.
Namna nyingine ya kutumia Lipstick
japo ime zoeleka lipstick hutumika katika midomo tu kuna namna nyingine ambapo lipstick ina weza kukusaidia
1) kuifanya kuwa highlighter
inaweza ikawa umesahau kubeba highlighter yako lakini kwenye pochi una lipstick yenye rangi ya highlighter labda rangi ya brown, unaweza kuitumia kama highlighter na ika kupa matokeo mazuri.
2)Lipstick kama eyeshadow
pia una weza kutumia lipstick kama eyeshadow na ika pendeza tu aina yoyote ya lipstick ina pendeza kuwa kama eyeshadow iwe lipstick kavu au ya mafuta lakini ni vizuri pia ukatumia zile rangi za kuonekana zaidi kama nyekundu, blue nk.
3) Lipstick kama tattoo
inaweza ikawa una penda tattoo lakini hupendi kuchora, unaweza kutumia Lipstick kwa kujichora vizuri kama tattoo na baadae ukatoa
Related posts
2 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More to that Topic: afroswagga.com/urembo/jiongeze-kujua-kiundani-kuhusu-lipstick/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on on that Topic: afroswagga.com/urembo/jiongeze-kujua-kiundani-kuhusu-lipstick/ […]