Kila asubuhi wanawake wengi yumkini na wewe unaesoma hapa unaweza kuwa mmoja wao huamka na kupaka vitu tofauti tofauti mwilini. Kile ambacho wengine hawaachi kufikiria ni nini wanaweka kwenye ngozi yao. Vipodozi vingi sana na bidhaa za utunzaji wa ngozi leo zimejaa viambata vyenye kemikali zenye kuharibu afya. Vingine hadi vimehusishwa na kansa.
Hadi sasa ongezeko la uhitaji na utolewaji wa elimu kuhusu vipodozi na ubora wake umeongezeka na kila mwanamke hata wewe unaesoma sasa hivi unatamani vipodozi natural. Baada ya kumaliza kusoma makala hii leo utaweza kujua Tofauti ya natural na organic na kati ya hizo ipi ni bora zaidi kuliko nyengine!

Tofauti kati ya kipodozi organic na kipodozi natural. Kwa haraka haraka unaweza ona kama ni kitu kile kile. Ila ukweli ni kwamba sio kila natural ni organic.
Kivipi?
Ili bidhaa iwe organic inatakiwa viambata vyake vitoke kwenye mashamba yanayolimwa bila mbolea za viwandani maana mbolea hizo huwa na kemikali. Kwa hio hufanya hivyo viambata visiwe organic.
Imekuja trendy watu wanasema wao wanatumia organic. Huku wakisahau kua yumkini nazi unayotengenezea mafuta nyumbani imeoteshwa na mbegu za kisasa au imewekwa mbolea ya kiwandani. Kwa maana nyingine ni kua natural peke yake haitoshi, Inatakiwa iwe organic ili iwe salama zaidi.
Bidhaa nyingi ambazo ni natural tunaziita natural kwakua hazina paraben kama kihifadhia bidhaa isiharibike (preservative) pia bidhaa inaitwa natural kwa sababu imetengenezwa na mimea na haijafanyiwa majaribio kwa panya.
Ila ukisikia na kuona kipodozi organic ujue hicho kimetengenezwa na malighafi ambazo toka shambani na chanzo chake hazijaongezewa chochote vile vile hazijawekwa kihifadhia bidhaa isiharibike. Ndio kusema Organic ni bora zaidi ya Natural kwa usalama wa matumizi yako.
Kwa upande wa bei na gharama organic ni bei au tuseme gharama yake iko juu zaidi ya ile natural, Natural bei au gharama yake ni nafuu kiasi japokuwa zote ni affordable inategemea na mhusika.
Baada ya kuelewa tofauti hizo, Hivyo basi utaamua mwenyewe kwa wewe ni bora organic au Natural!
Je wewe unatumia zaidi natural or Organic?
Related posts
1 Comment
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More to that Topic: afroswagga.com/urembo/jua-toauti-ya-vipodozi-organic-na-natural/ […]