Najua hapo ulipo unawaza na kufikiri je ni kweli nitaweza kutengeneza cream ya uso nyumbani kwangu na ikafanya kazi?
Kabla ya kujibu swali hilo nataka usome hadi mwisho kisha utajua kama ukitengeneza itafanya kazi au lah!
Kutengeneza cream nyumbani kwako ni njia nzuri ya kupunguza matumizi na kujiaminisha kwamba nitapata kitu natural hivyo nitaepukana na sumu za vipodozi vya madukani na gharama ya vipodozi.

Vile vile ni njia nzuri ya kutengeneza bomu ambalo hujui litakuripukia muda gani!
Usishtuke, bado nasisitiza usome hadi mwisho ili uweze kuelewa jee ni kweli cream utakayoitengeneza itafanya kazi!
Ili uweze kutengeneza cream na ifanye kazi unatakiwa kujua yafuatayo
:✔️Uwe unajua ni nini na nini kinaweza kuchanganywa bila ya kuharibu formula ya kitu husika na kwa kiasi gani!
✔️ Uwe unajua mazingira sahihi ya kutengeneza kitu husika. Unajua kwamba kemikali zingine huharibika tu zinapopata mwanga wa jua, au upepo?
✔️Uwe unajua namna sahihi ya kuzihifadhi mara tu unapomaliza kutengeza!
✔️Uwe unajua ni vimiminika gani vinahitajika katika kuchanganyia vitu husika, Jee unajua unatakiwa kutumia maji fresh au maji distilled ? Hii ni kwa sababu maji ya bomba bado sio pure kuweza kuchanganya na kutengeneza mchanganyiko ambao utataka udumu kwa muda kidogo, baada ya masaa machache huwa imeharibika na badala ya kupaka kitu salama unapaka bomu ulilitengeneza mwenyewe katika ngozi yako nzuri ya asili
Sio hayo tu, kuna mengine mengi ili kuhakikisha kitu bora kinagusa ngozi yako!
Sisi kama afroswagga tunakushauri kama unania, wazo ama unafanya mtindo huu acha mara moja kwa sababu madhara mengi yanayotokea kwenye ngozi yako leo sio matokeo ya kitu ulichokifanya jana ni masiku mengi huko nyuma.
Hapa tunamaanisha, Ukianza kufanya hivyo leo madhara yake huja kuonekana baada ya miaka kupita!
Kama unapenda home remedies
✔️Hakikisha unatengeza batch ndogo ndogo, unatumia unamaliza!✔️Unachanganya vinavyochanganyika kwa kufuata maelekezo husika.
✔️Ni bora zaidi kutumia remedy moja kama ilivyo zingine zinajitosheleza!✔️Na ni ukweli usiopingika huwezi Ku DIY kila kitu kwa usalama wa ngozi yako, vingine andaa bajet yako na ununue kutoka kwa genuine brand mana zipo kwa affordability ya kila mmoja!
Kingine, mara nyingi hizi home made cream hazinaga label, wala description zinazoonesha kilichotumika na kiasi chake, expire date wala siku iliyotengenezwa sijui unajihakikishiaje usalama wa kipodozi husika!
Ngozi yako ni nzuri sana hakikisha unachukua tahadhari katika kile kinachokuja karibu yako! Najua una hamu ya kutatua tatizo lako, lakini usalama wako ni muhimu zaidi usizidishe tatizo!
Jee hadi sasa utatengeneza face cream nyumbani?
©️binturembo
Related posts
3 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
We need to have some sort of bima ila for enjoyment. Yaani wanakata ka % ka mshahara kako unakua na card ukienda se… https://t.co/W9oDoaN2YY
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Here you will find 43979 additional Info to that Topic: afroswagga.com/urembo/jua-zaidi-kuhusu-kutengeneza-cream-nyumbani/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Info here on that Topic: afroswagga.com/urembo/jua-zaidi-kuhusu-kutengeneza-cream-nyumbani/ […]
… [Trackback]
[…] Read More to that Topic: afroswagga.com/urembo/jua-zaidi-kuhusu-kutengeneza-cream-nyumbani/ […]