Ingawa inawezekana wengine wakaona kitu cha ajabu, lakini ukweli ni kwamba kukata kucha kwa meno ni jambo linalofanywa na watu wengi.
Ni wazi kuwa si muda wote utakuwa na uhakika kuwa mikono yako ni safi na salama, hivyo inaweza kusababisha kujitafutia magonjwa ambayo yanaweza kuzuilika.
Kwenye upande mzima wa urembo, mtu anayeng’ata kucha anapoteza sifa yote ya kuitwa mrembo kutokana na kitendo hicho kuhusishwa na uchafu.
Wapo wanaofanya kwa makusudi na wengine hujikuta waking’ata vidole na kukata kucha bila kujitambua kama wanafanya kitendo hicho.
Mara nyingi hali ya kukata kucha bila kujitambua inatokana na mazoea ambayo mtu amejijengea hasa anapokuwa amezubaa na kukosa kitu cha kufanya hivyo kujikuta mikono yake ikielekea mdomoni.
Japokuwa wengi tunaamini mikono yetu, lakini kiafya kukata kucha kwa kutumia meno kunaweza kuleta madhara kadhaa ikiwamo kubeba vijidudu na kuviingiza mdomoni.
Bila kujitambua unaweza kujikuta ukivichukua vijidudu vinavyojificha kwenye kucha na kuvipeleka kwenye mdomo jambo ambalo linaweza kusababisha hatari

Hiki kitu kina waathirika wengi sana wake kwa wanaume wakubwa kwa wadogo. Tunaweza kudhani tu kuwa ni tabia mbaya au mazoea! La hasha kutafuna kucha za vidole vya mikononi ni tatizo la kisaikolojia linalomla mtu ndani kwa ndani kwenye ufahamu wake ambapo hupelekea viashiria hivi:-
-woga-mawazo/msongo wa mawazo-kutojiamini-fadhaa/sononi-kukosa la kufanya-taharuki-mapepe/restless mind-hulka ya kuiga
Hivyo ni viashiria vikuu vya mtafuna kucha na hili jambo hufanya bila kupenda ni involuntary action. Kuna baadhi hufanya wakiwa pekeyao kwenye upweke na wengine hufanya pindi anapokutana na mtu kwa mara ya kwanza ama hadhira.
Kwakuwa hili ni tatizo la kisaikolojia zaidi basi hata tiba yake ni ya kisaikolojia, hasa hasa
-councelling/ushauri nasaha-
kumjengea uwezo wa kujiamini mwathirika
-kutafiti kupitia yeye mwenyewe chanzo cha tatizo lake hilo na muda
Wengine hukutana na hii hali katika hatua fulani ya makuzi na ikipita tatizo hujitibu lenyewe!
Je una tatizo kama hili ama ndugu yako? Ama rafiki? Usikimbilie kwa mganga wa kienyeji utaambiwa una jini njaa..! Tiba unayo mwenye
©binturembo
Related posts
5 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Here you can find 76888 additional Information to that Topic: afroswagga.com/urembo/kungata-kucha-hupoteza-haiba-ya-urembo-wako/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Info here to that Topic: afroswagga.com/urembo/kungata-kucha-hupoteza-haiba-ya-urembo-wako/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Information here on that Topic: afroswagga.com/urembo/kungata-kucha-hupoteza-haiba-ya-urembo-wako/ […]
… [Trackback]
[…] Read More to that Topic: afroswagga.com/urembo/kungata-kucha-hupoteza-haiba-ya-urembo-wako/ […]
… [Trackback]
[…] Find More here to that Topic: afroswagga.com/urembo/kungata-kucha-hupoteza-haiba-ya-urembo-wako/ […]