Kupaka vipodozi pekee hakuwezi kukupa ngozi nzuri, bali pia unahitajika kuangalia unachokula pamoja na life style yako, ikiwa kuna hitilafu kwenye kimoja wapo basi utatumia nguvu nyingi sana kupata ngozi unayoitaka.
Ikiwa moja ya vitu ambavyo tunashauriwa kula kwaajili ya ngozi nzuri ni matunda na mbogamboga , inawezekana wewe si mpenzi wa vitu hivi basi unaweza kutengeneza juice ukanywa.
Moja ya juice ambayo inatajwa kuwa inafanya kazi vyema kwenye ngozi ni Juice ya carrot na manjano, je vinasaidiaje katika ngozi?
- Mizizi Ya Manjano / Manjano Mbichi
hufanya kazi kama moisturizer ya asili katika ngozi ambayo inaweza kusaidia kufanya ngozi kuwa laini na nyororo na kuzuia ngozi kuwa kavu. Ina anti-fungal, antibacterial na anti-inflammatory properties, yote ambayo zinamanufaa manufaa kwa watu wenye chunusi.
Inasaidia kukupa youthful skin na kupunguza kasi na dalili za kuzeeka na pia inaweza kusaidia kuzuia ngozi isizeeke mapema. Kwa wale walio na rangi tofauti mwilini, kunywa maji ya manjano kunaweza kusaidia kupunguza kuonekana kwa mabaka meusi kwenye ngozi na kuzuia ngozi kuwa nyeusi.
- Carrot
Carrot ina compound iitwayo beta carotene ambayo inaweza kusaidia kuimarisha afya ya ngozi. inaweza kusaidia kulinda ngozi dhidi ya miale ya UV (jua) na pia inaweza kusaidia kupunguza uharibifu wa ngozi na kuboresha mwonekano wake kwa ujumla. Ina vitamini V kwa wingi na ina antioxidants inavyoweza kusaidia kutengeneza tishu za ngozi zilizoharibika, huku pia ikisaidia kuboresha na kuipa mng’ao ngozi.
- Amla / Indian Gooseberry
Amla ina kiwango cha juu cha antioxidants ambayo inaweza kusaidia kuchelewesha dalili za kuzeeka kama mikunjo ya uzee na fine lines pia inaweza kuzuia kuzeeka mapema kwa seli za ngozi. Inaweza pia kusaidia kupunguza weusi katika ngozi.
Inaweza pia kusaidia kuboresha rangi, umbile,mwonekano wa ngozi, na hivyo kukupa mng’ao bora wa ngozi na mwonekano mzuri.

Viungo
- Carrot
- Manjano Mbichi
- Amla / Indian Gooseberry
- Maji
Namna Ya Kufanya
Osha karoti, mizizi ya manjano na amla kwa maji sadi ili kuondoa uchafu. Unaweza pia kuzilowesha kwa maji kwa nusu saa kabla ya kuzitumia.
Kata karoti na amla vipande vipande na uweke kwenye bakuli.
menya / toa ngozi manjano na ukate vipande vipande na uweke kando.
Weka karoti, manjano mbichi na amla pamoja na maji na uchanganye kwenye blender na u-brend mpaka vikiwa laini.
chuja na unywe unaweza kuweka kwenye fridge na ukainywa ikiwa ya baridi.
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…