Mwanamuziki, mtangazaji na muigizaji Lulu Diva ameonekana katika kipindi cha Mr. Right hivi karibuni akiwa anajipiga piga kichwa hii ni ishara ya kwamba wig yake ilikuwa ina muwasha na alikuwa ana jaribu kupunguza muwasho huo.
Kwa msanii mkubwa kama yeye hii hali haileti picha nzuri kwa maana moja ya sababu ya wig au nywele kuwashwa ina husishwa na nywele kuwa chafu, well baada ya kuona hili tumeona tuwaletee sababu na namna ya kuzuia aibu hii isitokee tena
Sababu za kwanini nywele yako inawasha
- Nywele zako za asili ni chafu
Mara nyingi tunaovaa wigs au kusukia weaving tunajisahau kwenye kusafisha nywele za asili kwa maana zinafichwa na hii husababisha uchafu kuzaliana ukakutana na joto basi lazima muwasho utokee.
- Una Mba
Mba ni tatizo kubwa kwa wengi wetu kama una mba na ukavaa wig lazima utapata miwasho mara mbili na ukiwa hujavaa wig au kushonea weaving.
- Una Allergy Na Shampoo / Vipodozi Vya Nywele Unavyotumia
Unapaswa pia kuzingatia ni bidhaa gani unatumia kwenye nywele zako na wigi yako kwani unaweza kuwa na mzio kwa baadhi ya viungo.3
- Hujakausha Nywele Zako Za Asili Vyema
Kama nywele zako za asili hazijakauka vyema unaweza kupata hisia ya kuwasha, pia. Kwa hivyo hakikisha unakausha nywele zako asili vizuri kabla ya kuvaa wigi kwa sababu unyevu kupita kiasi unaweza kusababisha miwasho.
- Ukosefu Wa Hewa Kati Ya Kichwa Chako Na Wig
Kama hakutokuwa na nafasi ya hewa kati ya wig na kichwa chako, kichwa chako hakiwezi kupumua hivyo kusababisha jasho na unyevu kupita kiasi na kuleta miwasho.
Nini Ufanye?
- Safisha nywele zako kabla ya kuvaa wig
- Tumia bidhaa za asili za nywele kusafishia nywele zako ili kuepuka allergy
- Hakikisha nywele zako za asili zimekauka vyema kabla ya kuvaa wig
- Tumia dawa za kutibu mba kabla ya kuvaa wig yako
- Chagua cotton wig cap ili nywele ziweze kupitisha hewa, na kuepuka ukaukaji wa ngozi na miwasho
- Nunua wig yenye quality nzuri
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…