Mafuta ya alizeti yanasifika kwa kuwa na fatty acids muhimu pia antioxidants muhimu zinazoweza kufaa katika kuzipa afya nywele zako pamoja na ngozi ya kichwa.
Mafuta ya alizeti yanasaidia watu wenye nywele kavu na ngozi ya kichwani inayowasha (itchy scalp), yatakusaidia kulaininsha nywele na kupunguza au kuondoa kabisa ile hali ya kichwa kuwasha.
Namna ya kufanya Treatment na mafuta ya alizeti pekee
Mahitaji
1. Mafuta ya alizeti
2. Chanuo au kitana kikubwa
3. Taulo lililowa maji ya moto/uvuguvugu
Jinsi ya kufanya
- Osha nywele zako ziwe safi, chukua mafuta ya alizeti ya kutosha paka kwenye nywele zako yakolee. Unaweza kuchana na kitana kikubwa ili kuyafikisha kwenye ncha za nywele zako.
- Jifunge kichwani taulo lako lililowa maji ya uvuguvugu ili kuzipa nywele unyevu na joto mafuta yaweze kupenya vizuri katika nwele zako.
Pia unaweza kuyatumia mafuta ya alizeti kwa kuchanganya na mafuta yako mengine ukayatumia kama base kwa kuwa ya bei rahisi, kisha unatia yale ya gharama kidogokidogo mfano unaweza kufanya mchanganyiko ufuatao:-
- Mafuta ya alizeti
- Castor Oil kidogo
- Almond oil kidogo
- Argan Oil kidogo au hata ya nazi
Mchanganyiko huu unaweza kuutumia kama treatment hapo juu au unaweza kuyapaka mara mbili kwa wiki kwa kuweka katika chupa yenye kipakio.
Related posts
2 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More on on that Topic: afroswagga.com/urembo/mafuta-ya-alizeti-kwa-ubora-wa-nywele-zako/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on to that Topic: afroswagga.com/urembo/mafuta-ya-alizeti-kwa-ubora-wa-nywele-zako/ […]