Majani haya yana kiasi kikubwa cha madini sulphur na Vitamin E ambazo ni asilia Kabisa na ni muhimu Sana katika urembo.Majani haya yana uwezo wa kupendezesha nywele zako pamoja na kuzifanya zikue vizuri zaidi, Pia yatapendezesha ngozi yako na kuiacha iking’aa pamoja kuondoa chunusi.
JINSI YA KUTUMIA MLONGE KATIKA NGOZI
Unaweza kutengeneza facial toner kwa kuchemsha majani yako ya mronge kisha uyaweke kwenye fridge tayari kwa matumizi, Jitahidi ndani ya siku 3 hadi 5 Utengeze Mpya.
➡ Unaspray usoni ama utapaka kwa kutumia pamba safi na baada ya robo saa utaosha kwa maji ya kawaida.
Pia unaweza kutengeneza mask ya mronge kwa ngozi nyororo kabisa
- Mahitaji
➡ unga wa majani ya mronge
➡ Unga wa mdalasini
➡Maziwa
➡Asali - Jinsi ya kufanya
✔ Changanya mahitaji yote pamoja kisha changanya vizuri.
✔Paka usoni na baada ya robo saa unaweza kunawa kwa maji ya kawaida.
JINSI YA KUYATUMIA KATIKA NYWELE ZAKO
Unaweza kutengeneza hair tonic kwa kutumia majani haya
✔ Chemsha majani yako Kisha yachuje na maji yake utaoshea nywele zako….
✔ Pia unaweza kuyatumia kama prepoo Yaani Kabla ya kuosha kwa shampoo, utasaga kwenye blender kisha ukamue juice yake na upake kwenye ngozi ya kichwa chako baada ya saa moja utaosha..
Unaweza pia kutengeneza mafuta kwa majani haya kwaajili ya ukuaji mzuri wa nywele zako.
- Mahitaji
➡Mafuta ya nazi pure/zeitun
➡Unga wa majani ya mronge…. - Jinsi ya kufanya
✔ Weka unga wa mronge kwenye bakuli safi kisha mimina mafuta yako na uyafunike.
✔ Baada ya siku 3 funua mafuta yako chuja vizuri ukiyafunua bila ya shaka.yatajitenga mafuta na makapi….
✔ Usichanganye na makapi chuja mafuta tu na yatakua tayari kwa matumizi.
✔Tumia mafuta haya kila siku ukihakikisha unayafikisha kwenye ngozi ya kichwa chako na ukimassage isipungue dakika 5 kila siku….
Je ulikuwa unafahamu namna ya kutumia mronge!? Tuambie kwenye comment hapo chini!
Imeandaliwa na Kuandikwa Na @bint_Urembo
Related posts
HOT TOPICS
Happiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/VZ1jH2zJUg
FollowHappiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/689j7Yjcn0
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
Feza Kessy Atuelezea Kuhusu Fashion & Style Zake
Feza Tadei Kessy ni Muimbaji, Muigizaji lakini pia ni mtunzi wa nyimbo lakini pia Fezza ni former beauty queen ambapo mwaka 2005 alikuwa Miss Dar City Centre, Miss Ilala & Miss Tanzania Runner up. Lakini pia alishawahi kuwepo katika Reality Tv Show – Big Brother Africa. Kwa…