Manjano ni kiungo kinacho tokana na mti uitwao curcuma longa, mti huu una patikana sana kusini mwa bara la Asia. Kiungo hiki kina tumiwa kwa namna nyingi una weza kutumia kama kiungio katika chakula lakini pia hutumika kama urembo na kina saidia sana.
manjano ina tumika kama bidhaa ya uzuri kwa muda sasa,ni njia rahisi na pia ina faida kubwa katika ngozi. Kabla ya kuwa na bidhaa za madukani bibi zetu walikua wakitumia manjano kutibia matatizo ya ngozi zao
Faida za manjano katika ngozi:
1) hutibu chunusi– manjano ina ufanisi mkubwa katika antiseptic ns antibacterial ambazo husaidia kupambana dhini ya chunusi na vidonda usoni na kuupa uso wako muonekano mzuri na mbichi manjano husaidia pia kupunguza mafuta usoni kwa wale wenye nyuso zenye mafuta.
Mahitaji
- Liwa- kijiko kimoja
- manjano- kijiko kimoja
- maji ya limao kiasi
changanya viungo hivi pamoja na kisha upake usoni na ukae navyo kwa muda usio pungua dakika kumi (10), kwa kuondoa chunusi changanya manjano na maji masafi na upake usoni ukae nayo kwa muda usio pungua dakika kumi na tano (15)
2) barakoa (mask) kwa wenye ngozi zenye mafuta – manjano yana manufaa katika ngozi zenye mafuta husaidia kupunguza mafuta na hio upelekea kupungua kwa chunusi usoni
Mahitaji
- maji ya machungwa
- liwa
- manjano
changanya changanyiko huo na upake usoni kisha ukae nao kwa muda wa dakika 10-15 kisha uoshe kwa maji ya vuguvugu.
3) barakoa (mask) kwa ngozi kavu- Kama una ngozi kavu , unaweza kufanya mask ya uso kwa kuchanganya 1 ute wa yai , 2 matone ya mafuta ya olive , maji ya limao na kuchanganya na manjano . Hii inaweza kutumika kwa maeneo yote kavu kama vile uso, shingo, elbows na magoti. ruhusu ikauke na kisha safisha na maji ya moto.
4) huondoa makunyanzi- Manjano ikichanganywa pamoja na viungo vingine,ina ufanisi katika kupunguza makunyanzi usoni . Unaweza kuandaa kwa kuchanganya unga wa manano pamoja na unga mchele na maziwa na juisi ya nyanya na kupaka juu ya uso wako na shingo kwa dakika 30 . Suuza na maji vuguvugu. Hii itapunguza makunyanzi katika ngozi na vile vile kuang’aza ngozi yako.
5) kuondoa stretch marks – manjano husaidia kung’aza au kufuta stretch marks changanya manjano na maziwa mgando/maziwa fresh/maji na kisha upake kwenye eneo lililo athirika.
Faida za manjano katika nywele
ukiachana na ngozi tu manjano pia husaidia katika ukuaji wa nywele pia hutibu baadhi ya matatizo kichwani
1) huondoa m’ba – changanya manjano na olive oil na paka kabla ya kwenda kuoga, kaa nayo kwa dakika 15 ndio uoshe
2) kupunguza kukatika kwa nywele – kukatika kwa nywele hutokana na kuumwa, kuto kula vizuri au msongo wa mawazo, kwa kuwezesha hili changanya asali na manjano na kisha uondoe kwa maji masafi.
Related posts
HOT TOPICS
We need to have some sort of bima ila for enjoyment. Yaani wanakata ka % ka mshahara kako unakua na card ukienda se… https://t.co/W9oDoaN2YY
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…